Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MSICHANA MIAKA 10 ADAIWA KUJARIBU KUJILIPUA KWA MABOMU AFGHANISTAN

 


Msichana Spozhmai aliyedai kulazimishwa kuvaa mabomu na kaka yake.
***
MSICHANA  mwenye umri wa miaka 10 aliyejulikana kwa jina mola la Spozhmai, nchini Afghanistan, anayedaiwa kutaka kujilipua kwa mabomu mbele ya kituo cha polisi, amekamatwa.
Akizungumza  na waandishi wa habari huko Lashkar Gah,  mji mkuu wa jimbo la Helmand, Spozhmai  alidai kwamba kaka yake ambaye ni kamanda wa wapiganaji wa Taliban alimlazimisha kuvaa koti maalum la kubebea  mabomu na kumtaka aende kwenye kituo kimoja cha polisi akajilipue.
Aliendelea kusema kwamba baada ya kumsimulia kaka yake juu ya kuchoshwa na vituko vya mama yake wa kambo dhidi yake, kaka yake huyo alimshawishi avae mabomu hayo aende kwenye kituo cha polisi cha wilayani Khanashin, kusini mwa nchi hiyo na abonyeze kidude cha kuyalipua.
“Nilivuka mto mmoja na baadaye nikaamua kulivua na kulitupa koti hilo.  Kaka yangu alikimbia na polisi wakanikamata,” alisema msichana huyo.
Habari kutoka televishni ya Tolo zimesema kilichokuwa kimetokea ni kwamba msichana huyo alishindwa kukibonyeza kidude cha kuyalipulia mabomu hayo.
Kumekuwa na habari kwamba Taliban wamekuwa wakiwatumia watoto katika kuweka mabomu kando ya barabara na kwa kujilipua, jambo ambalo wapiganaji hao wamelipinga.
NA: SKY NEWS
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top