MTOTO mmoja aliyetambulishwa kwa jina la Joyce Jeremia, 11,(pichani)
amejeruhiwa vibaya katika mapigano ya wa kulima na Wamasai ambao ni
wafugaji katika Kijini cha Laitini, Kiteto mkoani Manyara.
Aliongeza kusema kuwa baada ya uvamizi huo Wamasai hao walichoma
nyuma ambayo wazazi na watoto akiwemo yeye walikuwa akiishi lakini
Wamasai hao waliweza kufanya mashambulizi na kumuaa baba yake na
kumjeruhi mama yake huku akiona.
“Nilijaribu kumasaidia lakini nikakatwa panga kichwani na mama naye alikatwa mdomo na kukimbia kusikojulikana.
“Hadi hivi leo sina mawasiliano na mama yangu ambaye alikimbia na
wadogo zangu wawili ambao ni Furaha na Peter,” alisema mtoto huyo.
Mtoto huyo ambaye alipatwa na jeraha kubwa la kichwa amelazwa Moi
katika Wodi ya watoto na 8 akiendelea na matibabu huku akisaidiwa na
baba yake mdogo pamoja na shangazi yake.
Baba mdogo wa mtoto huyo alisema kuwa lengo la Wamasai hao lilikuwa
ni kuwaondoa wakulima hao ili waweze kuweka mifugo yao kwa ajili ya
kuchungia.
Aliongeza kusema kuwa alikuwa anapata taarifa kutoka kwa majirani
kuwa kaka yake aliyemtaja kwa jina la Kisuligwe Chilongola amefariki
dunia kutokana na vurugu za Wamasai.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, ACP Akili Mpwapwa alikiri kuwepo kwa mapigano hayo ya wakulima na wafugaji.
“Ni kweli mauaji yalitokea hadi sasa idadi ya waliouawa ni kumi na
majeruhi mmoja lakini kuhusu mtoto huyo hatukuwa na taarifa zake…
tunaendelea na uchunguzi ,” alisema Kamanda Mpwapwa.
>>GPL
Post a Comment