Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS ARUHUSU KUCHAPWA RASIMU YA KATIBA MPYA KATIKA MAGAZETI YA SERIKALI


Kifungu 20 (2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura 83, Toleo la 2013 inamtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchapisha kwenye
Gazeti la Serikali Rasimu ya Katiba ndani ya siku thelathini (30) baada ya kukabidhiwa rasimu hiyo na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue  inaeleza kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa 

Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, alikabidhiwa Rasimu ya Katiba tarehe 30 Desemba,  2013, na ataichapisha kwenye Gazeti la Serikali litakalotolewa Ijumaa, tarehe 24 Januari 2014.

Aidha, kifungu 22 (1) (c) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura 83,  Toleo la 2013, kinampa madaraka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushauriana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,  kuteua wajumbe 201 wa Bunge Maalumu la Katiba kutoka miongoni mwa majina  yanayopendekezwa kwao na makundi yaliyotajwa ndani ya Sheria hiyo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anakusudia kukamilisha uteuzi wa Wajumbe hao baada ya kushauriana na Rais wa Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar, mwanzoni mwa wiki ijayo na majina hayo kuchapishwa kwenye Gazeti  la Serikali kama kifungu 22 (3) cha Sheria iliyotajwa inavyomtaka kufanya.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
Dar es Salaam.
22 Januari, 2014
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top