Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SUMU YA CHUKI YAANZA KUSAMBAZWA CCM

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja akizungumza na wanachama. Picha na Mwandishi Wetu 
*************
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja ameonya baadhi ya viongozi wa chama hicho kuwajengea chuki wanachama kadhaa na viongozi kwa madai wako karibu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa.
Hatua ya Mgeja imekuja ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Geita, Joseph Kasheku ‘Msukuma’ kumkana na kumshutumu, Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM, Mgana Msindai kuwa anawalazimisha kuwa nyuma ya Lowassa wakati sivyo ilivyo.

Hata hivyo, Msindai alikanusha madai hayo kuwa hakuwahi kuwazungumzia wenyeviti wa CCM wa mikoa kuwa nyuma ya Lowassa zaidi ya kusema kuwa wanamuunga mkono katika masuala mbalimbali ya maendeleo.
Akizungumza katika mahojiano maalumu, Mgeja alimtetea Msindai kuhusu suala la wenyeviti wa CCM kuwa nyuma ya Lowassa katika urais. Alisema: “Nataka kutoa angalizo kwa viongozi ndani ya chama, Tanzania kwa ujumla, kumejitokeza tabia ya baadhi ya watu kuchukiana eti tu kwa sababu wako nyuma ya Lowassa,” alisema na kuongeza:
“Kumeanza watu kuchukiana, kuhukumiana kwa sababu uko karibu na Lowassa au kuwa na imani naye katika utendaji kazi wake, kumpenda na kumkubali mtu ni utashi wa mtu binafsi...tusihukumiane wala kuchaguliana marafiki,” alisema Mgeja.
Mgeja alisema: “Hakuna dhambi ya kumpenda au kumwamini Lowassa, lakini watu wanachukia, watu wananung’unika, wananuna haya yote ni majungu, woga, wivu na kutokujiamini. Inawezekana wanaofanya hivyo, wanatumwa na walio nyuma yao.
“Katika kipindi cha kuelekea uchaguzi, tusianze kusakana uchawi, muda ukifika, kila mtu atabebwa kwa sifa zake na atajibeba kwa umahiri wake.”
Mgeja alisema, kazi kubwa inayotakiwa kufanyika kwa wabunge, mawaziri na viongozi wa kada mbalimbali ni kukaa chini na kuwatumikia wananchi kwa kuhakikisha wanapata maji safi, dawa hospitalini na elimu kuliko kutumia muda mwingi kuangalia nani anampenda Lowassa.
“Kuna changamoto nyingi zinazowakabili wananchi na kila siku wanatuangalia viongozi, suala la vijana ni tatizo kubwa huduma za msingi kuliko kukaa na kuangalia Lowassa anafanya nini na yuko na nani, haileti tija hata kidogo,” alisema.
Mgeja aliwataka wanaCCM kutulia na kutafakari mambo ya maendeleo kwa kuwa hakuna mtu aliyejitangaza urais akiwamo Lowassa zaidi ya kuanzisha safari ya matumaini ambayo ndani yake kuna mafanikio katika elimu, huduma za afya, ajira kwa vijana na mambo mengi,” alisema.
Hivi karibuni, Msindai alikaririwa akisema: “Mimi ni Mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM, lakini sikuwahi kuzungumza kuwa wenyeviti wote wanamwunga mkono Lowassa katika Uchaguzi Mkuu 2015... kikubwa tulichozungumza ni kumuunga mkono katika safari yake ya mafanikio katika kuendeleza elimu, maji, ujenzi wa zahanati.”
Msindai alisema wanamwangalia Lowassa kutokana na uwezo wake katika kusimamia mipango yake ya maendeleo na zaidi katika kupigania elimu pana kwa Watanzania.
 
mwananchi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top