Meneja Mradi wa S.M.H RAIL
kutoka Malasya, V.Chalapathy pamoja na Meneja Ushauri wa Mradi wa
Kampuni hiyo, Wenceslaus Kaijage wakiwa mbele ya injini mpya 88U01
kabla ya kuanza safari ya majaribio kwenda Mkoani Dodoma.
Baadhi ya mafundi na wananchi wakiangalia injini mpya ya Treni mara baada ya kuwasili
stesheni ya Morogoro kutokea karakana ya TRL kabla ya kufanya safari ya
majaribio kwenda Dodoma.
Hapa tayari treni ikiwa imefunga mabehewa ya mizigo kuelekea Dodoma.
Ikitoka
karakana na behewa la mafundi tayari kuelekea stesheni ili kubeba
mahewa ya mizigo kwenda nayo Dodoma ikiwa safari ya majaribio. (PICHA/ MTANDA BLOG)
Na MTANDA BLOG, Morogoro.
KAMPUNI ya S.M.H.RAIL ya nchini Malasya leo imefanya safari ya majaribio ya injini mpya waliyoitengeneza kuanzia Stesheni ya Mjini Morogoro kwenda Mkoani Dodoma kwa mara ya Kwanza.
Majaribio
ya injini hiyo namba 88U01 imeboreshwa kutoka kwenye ile ya awali
iliyokua inafahamika kwa namba 8801 na kwa mujibu wa Meneja mradi wa
Kampuni hiyo Bw V .Chalapathy injini hii ni ya kisasa zaidi na inatumia
teknolojia ya kisasa ikiwa na nguvu ya HP 2300.
Meneja
huyo akiwa na timu ya mafundi ambao wameondoka na treni hiyo amesema
kwa majaribio injini hiyo itavuta tani 1125 za mzigo ingawa uwezo halisi ni kuvuta tani 1300 kwa mwendo kasi wa Km 50 kwa saa kulingana na uwezo wa reli za hapa nchini na kwamba kwa Malasya injini hii inaweza kwenda umbali wa Km 130 kwa saa kwa kua miundo mbinu ya njia za reli ni mizuri.
Akizungumzia katika
stesheni ya mjini Morogoro jaribio la kwanza lilikua ni kutembeza
injini yenyewe bila mzigo kwenda na kurudi Wilayani Kilosa na hili sasa
ni jaribio la pili na baada ya hapo wataikabidhi injini hiyo kwa TRL kwa
ajili ya usafirishaji wa abiria na mizigo.
Mshauri
wa Mradi huo Wenceslaus Kaijage alisema injini hiyo ina mfumo wa
udhibiti (Control unit) ambao kwanza unasaidia kuonyesha treni iko wapi
na kwa wakati gani njia nzima inapokua safarini na kwamba mfumo huo
unaruhusu kuisimamisha treni sehemu yoyote kwa kutokea stesheni au makao
makuu kwa kutumia mfumo wa kompyuta.
Mmoja
wa mafundi kutoka TRL ambao wako kwenye mradi huo wa kufufua injini
hizo ameidokeza majira kua vifaa vipya vilivyokuja kutoka Malasya ni
pamoja na injini yenyewe,Mashine ya mfumo wa upepo (Compressor) na
Jenereta na kwamba vitu vyote vilivyobakia ikiwa ni pamoja na bodi na
muundo wa injini hiyo vimefanyika katika karakana ya mjini Morogoro.
Stesheni Masta wa Mkoani Morogoro Flavian Nyawale
alisema kwa kua safari ni ya majaribio na bado injini hiyo bado iko
mikononi mwa Kampuni hiyo wao jukumu lao ni kuwapatia mzigo kulingana na
mahitaji ya majaribio yao ili kusoma tabia ya utendaji kazi wa injini
hiyo kwenye hatua za awali.
“Kama
injini haiwezi kufanya kazi kama inavyotakiwa huwezi kuipa namba kama
hii ya 88U01 na badala yake inarudia ile ile 8801 hii herufi U maana
yake ni Upgrading yaani imeboreshwa kutoka kwenye ile ya awali” alisisitiza Nyawale.
Post a Comment