.kitabu kipya chazua utata kuhusu mama mjamzito mvuta Sigara au Madawa ya Kulevya kuathiri hisia za kujamiiana kwa mtoto
.kitabu kinaonyesha maisha ya akina Mama Wajazwazito kuathiri kujamiiana kwa mtoto
.Sigara kusababisha mama kujifungua mtoto shoga-utafiti
Na Damas Makangale, MOblog kwa Msaada wa Mtandao
WANAWAKE
ambao hukabiliwa na matatizo hasa ya msongo wa mawazo wakati wa
ujauzito kuongeza nafasi ya mtoto wake kuwa shoga, kwa mujibu wa kitabu
kipya kilichozua utata huko ughaibuni.
Maisha
ya akina mama wajawazito huathiri kujamiiana kwa mtoto wake aliye
tumboni, kubadilisha homoni zao na malezi ya akili zao , ni moja ya
sababu ya kuzaa mtoto shoga.
Sigara
au kutumia madawa ya kulevya pia kunaweza kusababisha mtoto ambaye
kukua hadi kuwa shoga, kwa mujibu wa kitabu cha Uholanzi neuroscientist
cha Profesa, Dick Swaab.
Profesa
Swaab anaamini kwamba swala la uwezo wa mtoto wa kiume au wa kike
kujamiiana linaanzia tumboni kwa mama yake na haiwezi kubadilishwa ,
wakati wengine wanasema kuwa ni malezi ndio yanasababisha watoto kuwa
waathirika wa vitendo vya kishoga.
Katika
kitabu chake , Sisi ni akili zetu, yeye anaandika: ‘ Ingawa ni mara
nyingi kudhani kwamba maendeleo baada ya kuzaliwa ndio huathiri mwenendo
wa binadamu lakini pia muhimu kujua wakati wa maisha kabla ya kuzaliwa
kwenye chupa ya uzazi wa mama mjamzito,” amesema kwenye kitabu chake
Profesa, Swaab
Profesa
Swaab anasema kwamba maendeleo ya ubongo wakati wa ujauzito ni muhimu
katika kulinda afya ya uzazi kwa mtoto (Reproductive Health).
Profesa
Dick Swaab (juu), mwandishi wa kitabu Sisi ni akili zetu (chini),
anaamini kwamba kujamiiana mtoto ni kuamua tumboni na haiwezi
kubadilishwa.
Kwa
mfano, anadai kwamba madawa ya kulevya yalitumia kusaidia wakinamama
wajawazito mimba zisitoke (miscarriages) katika miaka ya 1940 na 1950
lakini baada ya kujifungua mashoga waliongezeka miaka hiyo.
Matumizi
ya sigara na sumu aina ya nikotini pia kuongeza nafasi ya mtoto wa kike
kuwa msagaji kwa kiasi kikubwa,” anasema Profesa huyo kwenye kitabu
chake.
Profesa Swaab, katika Chuo Kikuu cha Amsterdam, amechochea utata kwa maoni yake ya mimba kwa wakinamama kabla ya kujifungua.
Post a Comment