Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

DUNIA INA MAMBO NYIEEE .... WENGI WALITAMANI KANISA LA WALA NYASI

Na Mwandishi Wetu
BAADHI ya wananchi jijini Dar wamejitokeza na kuomba kujiunga na kanisa ambalo waumini wake wanakula nyasi.

Waumini wakila nyasi.
Kanisa hilo ambalo makao yake makuu ni Afrika Kusini linaloitwa Rabboni Centre Ministries gazeti hili liliandika katika toleo lake lililopita kuwa limeingia nchini na lipo maeneo ya Upanga jijini Dar.

Baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili mara baada ya kusoma habari hiyo walisema wanatamani kujiunga.
“Mimi nataka kujiunga na kanisa hilo kwa sababu tunataka wokovu,” alisema mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Amos.
Mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Frida Mandade alisema ana hamu ya kujiunga na kanisa hilo kwa sababu zake binafsi.
Kanisa la Rabboni Centre Ministries lina makao yake makuu Pretoria nchini Afrika Kusini na linaongozwa na mtu anayejiita Mchungaji na Nabii Daniel Lesego ambaye alilianisha mwaka 2002.
Wakati wa mfungo waumini wa kanisa hilo wametajwa kuwa huwa wanaishia kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo kwa imani kuwa Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni.

                gpl
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top