Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wachimbaji wacharuka, wateketeza kwa moto majengo ya Stamico

PICHA: MAKTABA

Vurugu kubwa zimetokea katika eneo la Mgodi wa Stamico uliopo Nyarugusu wilayani Geita, baada ya walinzi kumuua kwa kumpiga risasi mtu mmoja, hatua iliyowalazimisha wananchi kuvamia majengo ya Stamico na kuyachoma moto.
             
Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Leonard Paul, amethibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kwamba yeye na maofisa wake sasa wamefika katika eneo la tukio kwa ajili ya kudhibiti vurugu.
Alisema mpango huo utahusisha pia kuwasaka wanaojihusisha na vurugu.

Kwa mujibu wa shuhuda vurugu hizo, chanzo ni mmoja wa wachimbaji wadogo kupigwa kwa risasi na kuuawa wakati akiwa katika eneo la Mgodi wa Stamico.
Habari zilisema mgodi huo uko jirani na mgodi binafsi wa Buziba na kwamba hatua iliwafanya wachimbaji wadogo kupiga kelele na kuvamia eneo hilo na kisha kuchoma moto majengo ya mgodi huo.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, Alphonce Malingira, alisema baada ya wachimbaji wadogo kubaini kuwa mwenzao amekufa, walianza vurugu na kuvamia mgodi na kisha kuchoma moto majengo.
Pia walipora baadhi ya vitu zikiwemo kompyuta.
Akizungumza kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, Leonard Paul, alikiri kutokea kwa tukio hilo na kubainisha kuwa amelazimika kwenda katika eneo la tukio, kufuatilia kwa kina vurugu hizo.
“Kwa sasa siwezi kuzungumza lolote niko eneo la tukio na kazi ya uchunguzi imeanza ikiwa ni pamoja na kuwasaka waliohusika na vurugu, hivyo nitatoa taarifa baadaye,” alieleza.
Matukio ya polisi kuua wachimbaji yamekuwa yakitokea mara kwa mara migodini mkoani Geita.
MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top