Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAMA ASHA BILALI AJIUNGA NA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII WA PPF LEO KWENYE TAMASHA LA WANAWAKE NA AKIBA

 




 Mke wa Makamu wa Raisi Bi Asha Bilali akipata maelezo ya Kujiunga na Mfuko wa hifadhi ya Jamii wa PPF Kutoka kwa Meneja Mahusiano na Masoko wa Mfuko huo wa PPF Bi Lulu Mongere wakati alipofika katika banda la PPF kwenye Tamsha la Wanawake na Akiba katika Ukumbi wa Dar Live mapema leo



Mgeni rasmi wa tamasha la Wanawake na Akiba na ambae ni Mke wa Makamu wa Raisi Tanzania Bi Asha Bilali akijaza fomu ya Kujiunga na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PPF wakati alipotembelea banda la PPF kwenye Tamasha la wanawake na Akiba lililofanyika leo Katika Ukumbi wa Dar Live, Wanaoshuhudia ni Maafisa wa Mfuko wa PPF.


Mgeni rasmi ambae pia ni Mke wa Makamu wa raisi wa Tanzania Bi Asha Bilali akipigwa picha kwaajili ya kupata kitambulisho cha PPF mara baada ya kujaza fomu ya kujiunga na mfuko wa PPF mapema leo katika Tamasha la Wanawake na Akiba lililofanyika katika Ukumbi wa Dar Live mapema leo, Wanaoshuhudia pembeni ni Maafisa wa Mfuko wa PPF.



Mgeni rasmi ambae pia ni Mke wa Makamu wa Raisi wa Tanzania, Bi Asha Bilali akiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa mfuko wa hifadhi ya Jamii wa PPF wakati alipotembelea Banda la PPF leo katika tamasha la Wanawake na Akiba lililofanyika katika Ukumbi wa Dar Live mapema leo asubuhi.


Meneja Mahusiano na Masoko wa Mfuko wa hifadhi ya Jamii wa PPF Bi Lulu Mongere (Wa kwanza kulia) akitoa Maelezo Kwa wakazi wa jiji la Dar waliofika katika Banda lao Kwaajili ya Kujiunga na Mfuko wa Hiari kutoka PPF.


 Mkazi wa Jiji la Dar ambaye jina lake halikupatikana mara moja akifurahia kuchukua fomu ya kujiunga na Fao la Hiari kutoka Mfuko wa hifadhi ya Jamii  wa PPF mara baada ya kufika katika banda lao kwenye Tamasha la Wanawake na Akiba lililofunguliwa leo Katika Ukumbi wa Dar Live.Anayempatia Fomu ni Meneja Masoko na Mahusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PPF Bi Lulu Mongere


Meneja Mahusiano na Masoko wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PPF Bi Lulu Mongere akitoa maelekezo ya ujazaji wa fomu za kujiunga na Fao la Hiyari kwa wakazi wa jiji la Dar Waliofika katika banda lao lililopo kwenye Tamasha la Wanawake na Akiba lililofanyika Katika Ukumbi wa Dar Live.


 Wakazi wa Jiji la Dar Wakipata maelezo juu ya kujiunga na fao la hiyari kutoka kwenye mfuko wa hifadhi wa jamii wa PPF kutoka kwa Maafisa wa Mfuko huo wa PPF katika banda lao lililopo katika Tamasha la Wanawake na Akiba lililofanyika leo katika Ukumbi wa Dar Live.

Wakazi wa Jiji la Dar Wakifurahi pamoja na Maafisa wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Wa PPF mara baada ya Kujiunga na Mfuko huo wakati walipofika katika Banda la PPF kwenye Tamasha la Wanawake na Akiba lililofanyika katika Ukumbi wa Dar Live Mapema leo asubuhi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top