REAL
Madrid imefanikiwa kuingia Fainali ya Kombe la Mfalme baada ya usiku wa
jana kuizamisha Atletico Madrid kwa mabao 2-0 katika nusu Fainali ya
pili.
Shukrani
kwake Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo aliyefunga kwa penalti
mara mbili dakika ya saba na 16 na kufanya vigogo hao wa Hispania
wasonge mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-0.
Real sasa inaweza kukutana na barcelona katika fainali ya michuano hiyo Aprili 19 mwaka huu.
Lakini alitoka: Ronaldo alitoka uwanjani dakika ya 75 kumpisha kinda mwenye kipaji Jese
Post a Comment