Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SHEREHE ZA MIAKA 37 YA CCM KATA YA MABATINI WAITAKA SEREKALI KUKEMEA MAOVU

 

 

index

Mahmoud Ahmad Mwanza

Serekali imetakiwa kukemea maovu na ufisadi ili wananchi wawe na imani na chama chao na serekali iliyo madarakani kwani bila kukemea maovu yanayotokana ubadhirifu wa mali za serekali kwa waliopewa dhamana kujali mifuko yao badala yawalio wengi itazidi kukiumiza chama nakushindwa kukiamini kuwa kinatetea wanyonge.


Akizungumza kwenye kilele cha madhimisho hayo kabla ya kumkaribisha mwenyekiti wa chama wa kata hiyo katibu wa CCM wa kata ya Mabatini Gerald Mashala alisema kuwa kumekuwa na kawaida kwa watendaji wa serekali wasio waminifu kufuja mali za umma na kwataka viongozi wa chama hicho kuendelea kukemea maovu sanjari na ufisadi bila kmuonea haya yeyote kwani sisi ndio tumepewa ridhaa na wananchi kuongoza serekali



Mashala pia aliwataka wakazi wa jiji la mwanza na Tanzania kwa ujumla kuacha kutoa malalamiko pekee yake  kwani hayasaidi katika ujenzi wa taifa na badala yake wajitume kuliletea maendeleo taifa lao huu ndio uzalendo wa kweli malalamiko pekee hayasaidi tunatakiwa kukemea kwa nguvu zetu zote kila aina ya maovu na ufisadi.


” Utaifa kwanza ndio silaha yetu katika kujikomboa kutokana na maovu na ufisadi uliokithiti kwenye idara za serekali kwani malalamiko pekee hayatatasaidia kuondokana na maovu na ufisadi hapa tupige vita kwa nguvu zetu zote” alisisitiza Mashala.


Nae mwenyekiti wa ccm wa kata hiyo Yasiry Fuad aliwataka watanzania kuwa na mshikamano wakati huo tunapoelakea kwenye bunge la katiba nakuondoa itikadi za kisiasa na kuvaa utaifa kwani katiba si ya kisiasa inahitaji uzalendo wa hali ya juu katika kufikia mmustakabali wa taifa letu.

Fuad pia alisema kuwa suala la kukemea maovu ni jukumu letu sote na kuwataka watazania kujenga utamaduni wa kukemea maovu bila kujali itikadi za kisiasa kwani maendeleo hayana itikadi tuwe pia na tabia ya kujituma ilikujiletea maendeleo endelevu nakuacha malalamiko kwani serekali haiwezi kukuletea maendeleo nyumbani pako inainaleta maendeleo kwa jamii nzima.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top