Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BWAWA LA KIDUNDA KUTUMIKA KWA MAENDELEO YA TAIFA

IMG_0351

IMG_0264 (1)    
Baadhi ya washiriki wa warsha.
IMG_0278   Mkurugenzi Mtendaji wa DAWASA, Archad Mutalemwa akizungumza katika warsha.

IMG_0289Sekretarieti ya Warsha ya Wadau ya tathmini ya athari za Kijamii na   Mazingira.
IMG_0321
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akihutubia katika warsha.
IMG_0351
Wageni waalikwa wakiwa katika picha ya pamoja na Bodi ya DAWASA, watumishi wa Wizara ya Maji, DAWASA, DAWASCO na Bonde la Wami Ruvu.
IMG_0409Mwenyekiti wa mkutano, Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Bashir Mrindoko na Makamu Mwenyekiti ya Bodi ya DAWASA, Said El Maamry wakisikiliza mjadala katika  warsha hiyo.
……………………………………………………………………..
Warsha ya wadau ya kujadili taarifa ya tathmini ya athari za kijamii na mazingira ya mradi wa ujenzi wa Bwawa la Kidunda imefanyika jana katika Hoteli ya Nashera, mjini Morogoro.
Warsha hiyo imeshirikisha wadau wote wa sekta ya maji ngazi ya Serikali Kuu mpaka Serikali za Mitaa; ilijumuisha Wizara ya Maji, Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), Kampuni ya Maji Safi na  Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO), Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na viongozi wa mkoa wa Morogoro.
“Wazo la kujenga Bwawa la Kidunda kwa ajili ya matumizi mbalimbali, ikiwa pamoja na kuboresha huduma ya maji ya jiji la Dar es Salaam na miji ya Kibaha na Bagamoyo ni la muda mrefu. Hivyo, warsha hii ni mwendelezo wa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ili kuwezesha mradi wa ujenzi wa Bwawa la Kidunda”, alisema mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera.
Mkuu wa Mkoa aliongeza yapo manufaa mengi na makubwa yanayotokana na matumizi sahihi ya Bwawa la Kidunda, barabara na umeme baada ya ujenzi wa mradi huu kukamilika na kuleta maendeleo makubwa nchini.
“Bwawa la Kidunda ni mhimili wa vyanzo vya Ruvu Juu na Ruvu Chini, na ili uzalishaji wa maji kupitia mitambo ya Ruvu Chini uwe mzuri zaidi hatuna budi kujenga Bwawa la Kidunda. Aidha, kabla ya utekelezaji wake, ni muhimu kujadili athari zake kijamii na kimazingira na kupata ufumbuzi utakaopendekezwa na wataalamu”, alisema Mwenyekiti wa Bodi ya DAWASA, Hawa Sinare.
Pia, Mwenyekiti wa warsha hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Bashir Mrindoko alisema anawahakikishia wananchi kuwa athari zote na changamoto nyingine zitakazoainishwa na Mtaalamu Mshauri zitachukuliwa hatua sahii. Juhudi na tahadhari zimechukuliwa kuhakikisha kuwa kila mwananchi atakayeathirika anatendewa haki kwa mujibu wa sheria.
Lengo la warsha hiyo ni kutathmini athari za ujenzi wa barabara ya Ngerengere mpaka Kidunda, mtambo mdogo wa kuzalisha umeme kutoka Kidunda hadi Chalinze kijamii na kimazingira. Warsha hiyo ya siku moja iliandaliwa na (DAWASA) kushirikiana na Wizara ya Maji.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top