Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Hii ndiyo Jumla ya Watanzania waliohukumiwa kunyongwa China.

Kitanzi250114
Matukio ya kukamatwa kwa Watanzania nchini China huku wakihusishwa na biashara ya dawa za kulevya yamekua yakitangazwa mara kwa mara huku wengi wao tukipata taarifa za kuwa hukumu yao wamekuwa wakihukumiwa kunyongwa.

Image00002
Katibu Mkuu wa mambo ya Nje John Haule ametaja jumla ya watuhumiwa waliokamatwa kwa kesi ya madawa ya kulevya>>’Tuna Watanzania wengi tu ambao wapo kwenye magereza kule nchini China tumeshindwa kwa haraka haraka kupata idadi ya waliojihusha na shughuli ya dawa za kulevya’
Image00009
‘Katika Magereza ya China mpaka February tumepewa taarifa na Mamlaka za China kwamba wapo Magerezani Watanzania 177 na katika ya hao 15 wamehukumiwa kunyongwa kutokana na biashara hiyo ya dawa na kukamatwa na dawa hizo lakini niseme tu wenzetu wa Serikali ya China wanatuthamini sana kama sisi tunavyowathamini’
‘Lakini wenzetu wanathamini zaidi mahusiano yetu na ndiyo maana hata wale wachache Watanzania waliohukumiwa kunyongwa kutokana na makosa hayo waliyotenda kule hawajanyongwa mpaka leo na hatutegemei kama watanyongwa sana sana watafungwa kifungo cha maisha’.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top