Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MADEE AFUNGUKA BAADA YA WIMBO WAKE KUONDOLEWA NA BASATA KUWANIA TUZO ZA KILI 2014


Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA limeziondoa nyimbo tatu kwenye mchakato wa tuzo za muziki Tanzania, KTMA kwa madai kuwa zinakiuka maadili ya Kitanzania. Nyimbo hizo ni pamoja na ‘Nimevurugwa’ wa Snura, ‘Uzuri wako’ wa Jux na ‘Tema Mate’ wa Madee.

Madee akizungumza na Bongo5 leo baada ya kupata taarifa ya kuondolewa wimbo wake kwenye tuzo hizo, Madee amesema hajapendezwa na hatua hiyo.
 
“Sichukui hatua yoyote ila nawashangaa tu hao viongozi ambao wanahusika na mchakato mzima. Sisi tunaandika nyimbo ambazo vijana wetu wanazipenda,kwahiyo kama wameamua hivyo basi wawe wanatuandikia wao nyimbo,kwasasabu sisi tunawaandikia vijana wenzetu, sasa unakuta hao wanaoendesha mchakato ni wazee hawawezi kuchanganua maneno yetu,ifike time sasa wawe wanatuandikia mashairi,” amesema Madee.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top