Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KATIBU MKUU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, SAAZ SULULA, AKAGUA MIRADI YA HIFADHI YA ZIWA TANGANYIKA MKOANI RUKWA



Safari ya msafara wa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Saaz Sulula mwishoni mwa juma katika kukagua miradi inayofadhiliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira pamoja na wahisani wengine katika Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa haikuwa rahisi kutokana na kukabiliwa na changamoto ya barabara kutokana na mvua kubwa kunyesha na hivyo kupelekea magari ya mizigo inayokwenda nchi jirani za Burundi na DRC kupitia bandari ya kasanga kukwama na kuziba njia. Juhudi za ziada kwa kushirikiana na wananchi pamoja na mkandarasi anaejenga barabara hiyo ya Sumbawanga - Kasanga kwa kiwango cha lami zilisaidia katika kuhakikisha magari yote yaliyokwama pamoja na msafara wa katibu Mkuu yanavuka salama.   
 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Saaz Sulula (watatu kulia) akiwa na msafara wake wakielekea kagua wadi ya kujifungulia kinamama kijiji cha Samazi Wilayani Kalambo ikiwa ni sehemu ya mradi unaosimamiwa na mradi wa hifadhi wa ziwa Tanganyika uliopo chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira pamoja na miradi mingine ya ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya msingi Muzi na ujenzi unaoelekea kukamilika wa daharia (bweni) katika shule ya sekondari Kasanga. Katika msafara wake aliambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa (wa nne kulia)Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Saaz Sulula akizungumza na mhudumu wa afya katika wadi ya wazazi Samazi juu ya huduma na mahitaji ya kituo hicho kipya ambacho kinategemewa kuanza kazi siku za hivi karibuni.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais na msafara wake wakikagua vitanda kwa ajili ya wanafunzi pamoja na daharia katika shule ya  Sekondari Kasanga  Mkoani Rukwa. Mradi huo wa daharia (bweni) ni kwa ajili ya wanafunzi wa kike katika Shule hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Hassan Kimanta akimkaribisha Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Saaz Sulula katika Wilaya yake kwa ajili ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa soko la samaki la Kirando linalofadhiliwa na mradi wa usimamizi wa Ziwa Tanganyika uliopo chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Hassan Kimanta akimuonyesha Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Saaz Sulula (wa pili kushoto) sehemu inapojengwa gati kwa ajili ya kushushia samaki na abiria katika soko hilo pamoja na eneo linalojengwa kwa ajili ya kukaushia samaki wabichi. Kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Hassan Kimanta akimuongoza Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais na msafara wake katika kukagua ujenzi wa miundombinu inayoendelea kujengwa katika soko la samaki la Kirando Wilayani Nkasi Mkaoni Rukwa mwishoni mwa juma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Saaz Sulula akitoa baadhi ya maelekezo kwa mkandarasi wa Soko la Samaki la Kirando ambae pia anajenga Gati linaloonekana kwa ajili ya kuunganisha huduma katika soko hilo na bidhaa za samaki zinazotoka  ziwani (Ziwa Tanganyika).  
Gati linaloendelea kujengwa kwa ajili yakuhudumia soko hilo la samaki la Kirando wilayani Nkasi.(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @ rukwareview.blogspot.com)
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top