Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KATIBU MKUU WA CCM, NDUGU KINANA ALIVYOFUNGA KAMPENI ZA UCHAGUZI JIMBO LA KALENGA .... AACHA HISTORIA JIMBO LA KALENGA




 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kwa tiketi ya chama hicho,Ndugu Godfery Mgimwa,wakati wa mkutano wa kufunga kampeni katika jimbo la Kalenga,katika kijiji cha Kidamali kata ya Nzihi,Iringa Vijijini mkoani Iringa.Uchaguzi wa jimbo la Kalenga unafanyika kesho siku ya jumapili,Machi 16,kuziba pengo la aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo,Waziri wa Fedha na Uchumi,Marehemu Dk.William Mgimwa.


 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akihutubia Wananchi wakati wa kufunga Kampeni za Uchaguzi wa jimbo hilo jioni ya leo,katika kijiji cha Kidamali,kata ya Nzihi Iringa vijijini.


 Mkutano wa kufunga kampeni ukiendelea kwenye kijiji cha Kidamali kata ya Nzihi jioni ya leo.


  Mgombea Ubunge jimbo la Kalenga (CCM),Godfrey Mgimwa akimtambulisha mke wake,Bi.Robby Mgimwa kwa wananchi wa kijiji cha Kidamali kata ya Nzihi,ambako kumefanyika mkutano wa kumfunga kampeni jioni ya leo.








  Mgombea Ubunge jimbo la Kalenga (CCM),Ndugu Mgimwa akiwa amebebwa juu juu na Wafuasi wa chama hicho,mara baada ya kuwasili kwenye Mkutano wa kufunga kampeni za cha hicho,zilizofanyika katika kijiji cha Kidamali,Kata ya Nzihi,Iringa vijijini.


 Mbunge wa jimbo la Ludewa,Mh.Deo Filikunjombe akihutubia mbele ya wananchi katika suala zima la kumuombea kura Mgombea Ubunge wa CCM,Jimbo la Kalenga,Ndugu Godfrey Mgimwa jioni ya leo kwenye kijiji cha Kidamali Kata ya Nzihi Iringa vijini. 


Mke wa Mgombea Ubunge Jimbo la Kalenga kwa tiketi ya chama cha CCM,Bi Robi Mgimwa akiwa amepiga magoti mbele ya wananchi waliokuwa wamefika kwenye mkutano wa mwisho wa kampeni za chama hizo,akimuombea kura mumewe ili ashinde.


 Wakina dada wakifuatilia mkutano huo 


 Wadau nao walikuwepo.


  Wananchi mbalimbali wakiwa kwenye mkutano wa kampeni ya lala salama ya CCM,jioni ya leo kwenye kijiji cha Kidamali,kata ya Nzihi Iringa Vijijini. 


 Wanahabari wakiendelea kuchukua matukio mbalimbali kwenye mkutano huo wa kampeni.


 Wakazi wa kijiji cha Kidamali kata ya Nzihi wakishangilia jambo.


 Niabu Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Mwigulu Nchemba akimnadi na kumwombea kura mgombea wa Ubunge wa CCM,jimbo la Kalenga,Ndugu Godfreya Mgimwa katika kijiji cha Kidamali kata ya Nzihi,katika mbio za kufunga mkutao wa Kampeni jioni ya leo

 Mke wa Mgombea,Bi Robby Mgimwa akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana,kushoto ni Katibu wa CCM mkoa Iringa,Ndugu Hassani Mtenga.


 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza jambo na Mhadhiri wa chuo cha Tumaini  na Mtangazaji wa Radio One na ITV,Godfrey Gondwe.


Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Kidamali,Kata ya Nzihi,Iringa Vijijini jioni ya leo,kabla ya kuhutubia kufunga kampeni za chama hicho,kupisha uchaguzi unaotarajiwa kufanyika hapo keshoi katika jimbo la Kalenga.


Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Mgombea Ubunge jimbo la Kalenga (CCM),Ndugu Mgimwa wakiwapungia mikono wananchi jioni ya leo kwenye mkutano wa kufunga kampeni za chama hicho.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top