Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

LUDEWA WAMPONGEZA RAIS DKT. KIKWETE

 


Na  Francis Godwin Blog 
IMG_2099WANANCHI  wa Ludewa  mkoani  Njombe  wamempongeza  Rais Dr Jakaya Kikwete kwa hatua  yake ya  kuwashirikisha  wananchi wa maeneo husika katika suala la utatuzi wa mgogoro wa mpaka  kati ya Tanzania na Malawi
 
Hatua  ya  wananchi  hao  kumpongeza  Rais  Dr Kikwete  imekuja  huku  ikiwa ni  siku  tatu zimepita  toka  mbunge wao  wa jimbo  la Ludewa Deo Filikunjombe ,mbunge wa jimbo la Kyela Dk. Harrison Mwakyembe na mbunge wa jimbo la Mbinga  Magharibi John Komba  kurejea nchini  kutoka Malawi  katika  kikao  cha usuluhishi  wa mgogoro  wa mpaka kati ya Malawi na Tanzania
 
Wakizungumza na  mwandishi  wa habari hizi wananchi hao  akiwemo Yohana  Haule  walisema  kuwa  hatua  ya  Rais Kikwete  kutumia  wananchi  wenye  kushughulikia  suala  hilo  ni hatua ya  kupongezwa  kwani wabunge hao  ni wawakilishi wa  wananchi hivyo kila kinachoendelea kitawafikia mapema  wananchi  wa maeneo ya mpakani Malawi na Tanzania.
 
Haule alisema  kuwa  imani na matumani  ya  wana Ludewa ni kuona mbunge  wao amewawakilisha  katika  suala hilo na  kuwa  hawana  shaka na uwakilishi  wake na wanaamini  watapewa mrejesho  wa  kila kinachoendelea  katika  suala  hilo.
 
Hivyo  alisema  kwa  sasa hofu  ambayo awali  wananchi wa kando ya  ziwa Nyasa  walikuwa nayo  juu ya mgogoro  huo wa mpaka kati ya  Tanzania na Malawi  imeanza  kutoweka  kutokana na mbunge  wao Filikunjombe kuzunguka maeneo  yote ya Mwambao na  kufanya  mikutano na  kuwaondoa hofu  juu ya  hilo.
Huku Sarah Haule  mbali  ya  kumpongeza  Rais  Kikwete kwa  hatua  hiyo  pia  alimpongeza mbunge  Filikunjombe kwa jitihada mbali mbali  za kuwaletea  maendeleo  wananchi  wa Ludewa huku  akimtaka  mbunge   huyo kuendelea  na msimamo  wake  katika kuwawakilishi  wana  Ludewa bungeni .
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top