"Ni vyema
 tukatambua kuwa Watanzania ni wapenda amani, hivyo wasingependa kuona 
kukijitokeza tofauti kati ya wajumbe wa Bunge hilo.
Dar es 
Salaam. Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam, 
Mwadhama Kardinal Pengo amesema shughuli za mchakato wa Katiba zifanyike
 kwa amani na kwamba ziwalinde Watanzania katika umoja na mshikamano 
waliyokuwa nao.
Pia, 
amewataka wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kuweka masilahi yao kando na
 kutanguliza masilahi ya taifa kwa faida ya Watanzania.
Akizungumza
 jana kwenye uzinduzi wa Katisa Katoliki Magomeni, Kardnali Pendo 
alisema ni vyema viongozi wakafahamu kwamba Watanzania ni watu 
wanaopenda amani, na kwamba yeye angepAenda kuona amani iliyopo inadumu.
Alisema: "Niseme kwamba, shughuli za mchakato wa kuandika Katiba Mpya zifanyike kwa amani."
Aliongeza:
 "Ni vyema tukatambua kuwa Watanzania ni wapenda amani, hivyo 
wasingependa kuona kukijitokeza tofauti kati ya wajumbe wa Bunge hilo,"
Alisema 
kama tunataka nia ni kupata katiba bora, ni lazima wajumbe wabunge la 
Maalum la Katiba kuweka masilahi ya yao kando na kuangalia yale ya taifa
 kwa faida ya Watanzania wote.
Alitoa 
mfano kwa baadhi ya vingozi wa nje ya nchi wanavyotambua mchango wa Baba
 wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa kuwa ni mtu aliyependa amani, 
umoja na mshikamamno.
Alisema 
leo (jana) alifuatilia vyombo vya habari na kusikia kuwa Rais wa 
Zimbabwe (Robert Mugabe) akimuelezea Mwalimu Nyerere kama kiongozi 
shupavu aliyeweka misingi ya amani Tanzania kwa kuwa alikuwa mpenda 
amani.
Naye, 
Paroko wa Kanisa hilo Joseph Matumaini alisema Kanisa hilo limejengwa 
kwa ghalama ya Sh1.25 bilioni fedha ambazo zimetokana na michango ya 
waumini wao.
Alisema: 
"Kanisa hili limejengwa kwa jitihada za waumi kwa kujitolea, na kwamba 
tunawashukuru wote kwa kuijenga nyumba ya mungu,"
Alisema Kanisa hilo lina uwezo wa kuchukua waumini 1500.
Chanzo, mwananchi.

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment