Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI WILAYANI RUNGWE YABAINI USAFIRISHAJI WA POMBE KWA NJIA ZA PANYA TOKA MALAWI


Na Ibrahim Yassin,Rungwe

SERIKALI wilayani Rungwe mkoani Mbeya imebaini mbinu mpya za usafirishaji wa pombe haramu za viroba  toka nchini Malawi inazofanywa na wafanyabiashara wasio waaminifu ambao husafirisha viroba hivyo kutoka Malawi kupitia njia za panya zilizopo boda ya kasumulu wilayani Kyela kwenda mikoani.
Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela alisema kuwa mbali na kupiga marufuku uingizaji wa pombe hizo nchini lakini bado kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakibuni mbinu mpya ya kusafirisaha pombe hizo haramu ambazo tayari wamezibaini.
Alisema kuwa katika uchunguzi uliofanywa na kamati yake ya ulinzi na usalama juu ya kuzibaini njia hizo tayari walikwisha wabaini wafanyabiashara ambao walikuwa wakisafirisha pombe hizo katika mifuko ya sarfeti na juu yake wamekuwa wakiweka nafaka ili wasibainike na kwamba njia nyingine hutumiwa na akina mama ambao hupakata viroba hivyo ambavyo huviviringisha kwenye vitenge mithiri ya mtoto bila ya kugundulika.
Aliongeza kuwa mbali na maafisa wa TFDA kuwatoza faini wamiliki wa magari yanayokamatwa yakiwa yamebeba na kusafirisha pombe hizo   pamoja na kutaifisha pombe hizo haramu kwa wafanyabiashara ambao hukamatwa lakini haijasaidia bado pombe hizo zinazidi kuingia nchini kupitia boda hiyo ya kasumulu iliyopo wilayani Kyela.
Kutokana na hali hiyo mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa alikwisha keti na kamati ya ulinzi na usalama na kujadili namna ya kukomesha na kudhibiti usafirishaji huo kwa kutunga sheria kandamizi itakayowabana wamiliki wa magari wanaopewa tenda ya kusafirisha bidhaa hizo haramu na wafanya biashara wenyewe kwa lengo la kuokoa nguvu kazi ya Taifa la vijana ambao wamekuwa wakipata madhara juu ya matumizi ya pombe hizo.
Alizitaja sheria hizo kuwa ni kutaifisha gari au pikipiki ambayo litakamatwa ikiwa limebeba pombe hizo ikiwa ni pamoja na kuwapeleka mahakamani wafanyabiashara watakao kamatwa wakiwa wanasafirisha au kuuza pombe hizo haramu zilizopigwa marufuku na Serikali.
Meela aliongeza kuwa katika jitihada zao za awali za uthibiti wa pombe hizo  wamefanya utafiti wa miezi mitatu na kubaini kuwa   wamefanikiwa kwa asilimia 80 kuthibiti matumizi ya pombe hizo kwa wilaya ya Rungwe na Kyela na kuwa tayari ajali za barabarani zimepungua kwa madereva wa badabada waliokuwa wakitumia pombe hizo wakiwa kazini ikiwa ni pamoja na kupunguza vifo vya vijana waliokuwa wakitumia vinywaji hivyo.
Alisema kuwa katika operesheni waliyoifanya kwa miezi mitatu iliyopita tayari wamefanikiwa kukamata katoni 3,000 ambazo zitateketezwa mwishoni mwa wiki hii na kuwafikisha mahakamani wafanyabiashara 6 waliokamatwa wakati wakisafirisha pombe hizo na kuwa sheria itafuata mkondo wake ili iwefundisho kwa wengine ambao watakaidi amri ya serikali ya upigaji marufuku pombe hizo hatarishi kwa maisha ya wanadamu.
Aliyataja madhara wanayoyapata wanadamu pindi watumiapo pombe hizo kuwa ni kuishiwa nguvu za kiume,kukosa hamu ya kula,tendo la ndoa,kuungua ini,kuchanganyikiwa na kupoteza kumbukumbu na hatimae kifo,na kwamba tayari ameiagiza kampuni ya kizalendo inayotengeneza pombe za konyagi isambaze katika wilaya hizo kwa kuwa hazina madhara zimedhibitiwa na TBS.
Aliongeza kuwa mpango mkakati waliupanga katika wilaya yake kwa kushirikiana na viongozi wa wilaya ya Kyela ambayo ndiyo uchochoro wa kupitishia pombe hizo ni kuanza operesheni ya pamoja ya duka hadi duka na kuweka maafisa wa polisi katika njia zote za panya zilizopo kwenye kivuko cha mto songwe unaotenganisha nchi ya Tanzania na Malawi kwa lengo la kutokomeza kabisa matumizi ya pombe hizo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top