Bi. Jacqueline Mkindi akisisitiza Jambo wakati wa hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo hayo
Bi. Jacqueline Mkindi akisisitiza Jambo wakati wa hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo hayo.
Na. Mwandishi Wetu
KATIKA kuhakikisha kwamba thamani ya mazao ya horticulture(maua, na mboga mboga)  nchini Tanzania inapanda na hivyo kupata masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi, Tanzania Horticultural Association
(TAHA), imeamua kuendeleza harakati hiyo kwa kutoa mafunzo ya misingi bora ya kilimo kwa mazao hayo kwa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

Mafunzo hayo ya siku tatu yaliyofanyika hivi karibuni wilayani Makete ambayo yanalenga kutoa misingi fasaha na mbinu zinazotumia teknolojia rahisi za kisasa ili kuongeza tija na thamani kwenye mazao ya horticulture yamezinduliwa hivi karibuni na Mkurugenzi wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Mwanamakala Mohamed Killo, sambamba na Mkurugenzi Mtendaji wa TAHA, Bi. Jacqueline Mkindi.
Aidha, mafunzo hayo yanayoendeshwa na mtaalamu wa kilimo cha mazao ya horticulture wa TAHA, Manfred Bitala, katika ukumbi wa klabu ya jeshi la JKT Ruvu, yanafanyika kwa nadharia na vitendo ambapo maafisa wa Jeshi waliopata fursa ya kuhudhuria mafunzo hayo watajifunza kwa vitendo mbinu hizo kwenye moja ya mashamba yaliyo katika eneo la jeshi hilo.
Mkurugenzi wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Mwanamakala Mohamed Killo akizungumza na washiriki wa mafunzo
Mkurugenzi wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Mwanamakala Mohamed Killo akizungumza na washiriki wa mafunzo.
Awali alipokuwa akifungua mafunzo hayo siku ya Jumatatu Mkurugenzi wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Killo, alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuleta mapinduzi ya kilmo bora cha mazao ya horticulture yenye kukidhi viwango vyenye ubora wa kimataifa na hivyo kuvutia soko na uwekezaji kwenye sekta hiyo nchini.
“Uzoefu wa masuala ya msingi ambayo wataalamu wa Jeshi letu wataupata utakuwa chachu ya kuleta mapinduzi ya kilimo bora cha mazao ya horticulture yenye kukidhi viwango vya ubora wa kimataifa na hivyo kuvutia wawekezaji na soko nchini,” alisisitiza Brigedia Killo.
Akizungumza wakati wa hotuba yake ya ufunguzi, Mkurugenzi Mtendaji wa TAHA, Bi. Jacqueline Mkindi,   alibainisha kuwa licha ya Jeshi hilo kupata mafanikio katika kuzalisha maelfu ya tani za mazao ya horticulture kila mwaka, jitahida zaidi za jeshi hilo zinahitajika ili kuongeza viwango vya uzalishaji vinavyokidhi masoko ya kimataifa kila mwaka.
Mkurugenzi wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Mwanamakala Mohamed Killo akifurahia jambo wakati alipokuwa akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo hayo katika ukumbi wa JKT CLUB RUVU
Mkurugenzi wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Mwanamakala Mohamed Killo akifurahia jambo wakati alipokuwa akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo hayo katika ukumbi wa JKT CLUB RUVU.
Bi.Mkindi, aliongeza kuwa Tanzania inayo fursa nyingi za uzalishaji na uwekezaji katika sekta ya mazao ya horticulture ingawa fursa hizo zinaendelea kubaki wazi hadi sasa pasipo kutumiwa ipasavyo.
Mkurugenzi huyo wa TAHA, ameto wito kwa jeshi hilo kupitia mafunzo wanayoyapata kuwa mfano kwa kuzitumia fursa za uwekezaji na masoko ya mazao ya horticulture nchini.
Katika kipindi cha mwaka uliopita Jeshi la JKT-Ruvu lilizalisha mzao mbalimbali kwenye shamba la majaribio ikiwemo; kilo 22,797 za (mchicha), kilogramu   24,175, (nyanya), kilogramu 31,438 (matango) ni kilogramu 12410 (bilinganya) na Vitunguu kilo 2211.
Ndugu Manfred Bitala mtaalamu wa ufundi wa kilimo cha mazao ya horticulture wa TAHA akitoa mwongozo wa mafunzo ya kilimo cha mazao ya horticulture
Ndugu Manfred Bitala mtaalamu wa ufundi wa kilimo cha mazao ya horticulture wa TAHA akitoa mwongozo wa mafunzo ya kilimo cha mazao ya horticulture.
Washiriki wa mafunzo wakimsikiliza Mkurugenzi wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Mwanamakala Mohamed Killo
Washiriki wa mafunzo wakimsikiliza Mkurugenzi wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Mwanamakala Mohamed Killo.
Mkurugenzi wa TAHA katika picha ya pamoja na maafisa wa Jeshi la JKT wanaohudhuria mafunzo ya uzalishaji wa mazao ya horticulture yenye tija na thamani
Mkurugenzi wa TAHA katika picha ya pamoja na maafisa wa Jeshi la JKT wanaohudhuria mafunzo ya uzalishaji wa mazao ya horticulture yenye tija na thamani.