Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wafanyabiashara na wachimbaji Tanzania walifikia soko la madini Kimataifa

 


1 (7)Wafanybiashara na Wachimbaji waliowakilisha wenzao katika Maonesho ya 53 ya Bangkok Gems and Jewelry Fair’ wakiwasikiliza wageni waliotembelea banda la Tanzania kuona aina mbali mbali za madini ya Vito na Usonara yaliyowasilishwa katika maonesho hayo.
2 (5)Mthamini wa madini kutoka idara ya Uthamini wa madini ya Almas (TANSORT) Bw. Edward Rweymamu (katikati), akiwaeleza jambo wageni waliotembelea banda la Tanzania katika maonesho hayo. Wanaoshuhudia wa kwanza kushoto ni Mratibu kutoka Kituo cha ‘Tanzania Geomological Center’ (TGC), Bw. Musa Shanyangi na wa kwanza kulia ni Mthamini wa Madini kutoka Idara ya  uthamini madini ya almsi  (TANSORT), Wizara ya Nishati na Madini Bibi. Teddy Goliama.
3 (4)Mwandishi wa habari hii (Kushoto) Asteria Muhozya, akifanya mahojiano na wafanyabiashara wa madini walioshiriki maonesho ya Vito na Usonara ili kutaka kujua namna walivyofaidika na ushiriki wao katika maonesho hayo. Anayeongea ni Bw. Jeremiah Simioni Mfanyabiashara kutoka Kampuni ya Tom Gems na katikati ni Mfanyabiashara Mhe. Dorah Mushi kutoka Kampuni ya H.B Mining Company.

…………………………………………………………………..
Na Asteria Muhozya, Bangkok
Wafanyabiashara na wachimbaji wa madini Tanzania wameelezea kufurahishwa na ushiriki wao katika maonesho ya 53 ya madini ya vito na usonara, Bangkok, kutokana na kupata fursa ya kulifikia soko la madini kimataifa.
“Wachimbaji wa madini ya vito na usonara, watarajie kupata masoko ya madini yao nje. Wananunuzi wa bidhaa zetu wapo na wana imani kubwa na madini yetu. Jambo kubwa tulilolihitaji ilikuwa kujua masoko na namna ya kupata taarifa mbalimbali. Tunafurahi kwa hilo, tumefanikiwa.  Amesema Mwenyekiti wa Kamati ya Madini ya Vito Tanzania, Bw. Gregory Kibusi.
Aidha, Aliongeza kuwa, ushiriki wake katika maonesho hayo, umewawezesha kupata sehemu ambazo zitawasaidia wachimbaji kupata taarifa mbalimbali, ikiwemo taarifa za bei za madini hali ambayo itawawezesha kupata taarifa sahihi tofauti na awali, ambapo walikuwa wakizipata kutoka vyanzo visivyo rasmi. Hivyo, amewataka wachimbaji kufanya maandalizi mazuri kwa ajili ya maonesho ya madini ya vito na usonara yanayofanyika kila mwaka jijini Arusha.
Akizungumzia namna alivyonufaika na maonesho hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya madini ya H.B Bw. Harry Mushi, alieleza kuwa, maonesho hayo, yamewasaidia kujua nafasi zao kibiashara. Vilevile, ameongeza kuwa, maonesho hayo yamewasaidia kujua aina za madini zinazotakiwa kuwasilishwa kwenye maonesho ya kimataifa, na umuhimu wa kuzingatia ubora wa madini.
“Tumegundua wafanyabiashara wa madini Tanzania tunahitaji kujipanga ili kuliteka soko la kimataifa. Tumejifunza umuhimu wa kukata madini. Madini tunayo na ni bora sana. Wachimbaji wanatakiwa kuyaongezea thamani madini yao. Jambo hili ni muhimu sana, tunahitaji kujipanga.” Ameongeza Mushi.
Kwa upande wake mfanyabiashara wa madini kutoka kampuni ya H.B Mining, Mhe. Dorah Mushi, alieleza kuwa, ipo haja kwa Watanzania kuinuka kutokana na ukweli kwamba, Tanzania inayo hazina kubwa ya madini ya aina mbalimbali takriban katika kila Mkoa kutokana na kwamba, maonesho ni njia mojawapo ya kusaidia kujenga mtandao wa kibiashara.
Aidha, ameiomba Serikali kuwasaidia wananawake walioko katika sekta ya uzalishaji wa madini ili waweze kufahamu fursa zilizopo na kujua namna ya kuzitumia. Ameongeza kuwa, wapo wanawake wengi katika sekta hiyo ambao wameshindwa kufaidika na sekta hiyo kutokana na ukosefu wa elimu.
 “Madini ni maisha, ni biashara, ni ajira. Kina mama litambueni hili, jiingizeni katika sekta hii soko la kimataifa lipo.  Nimeshiriki hapa Bangkok kwa mara ya kwanza Sitaki kukosa tena maonesho kama haya. Nimejifunza mengi ikiwemo namna ya kuuza madini. Serikali wasaidieni wadau wa madini , hasa kina mama , wafumbueni  macho”.  Amesema Mhe. Dora Mushi.
Wakati huo huo, mfanyabiashara wa madini na Afisa Masoko wa kampuni ya Tom Gems, Bw.  Jeremiah Simioni, aliishukuru Serikali ya Tanzania   kutokana na  kuwa   na uhusiano mzuri na nchi ya Thailand kutokana na kwamba, ushiriki wao katika maonesho hayo, umewafungulia mipaka ya ufahamu kuhusiana na biashara ya madini ya vito na usonara katika ngazi za kimataifa.
“Nataka kuwa balozi kwa wenzangu baada ya kushiriki maonesho haya. Nataka kuwaambia wenzangu fursa zilizopo kimataifa na namna wanavyopaswa kuzitumia. Naishukuru sana Wizara  na idara ya uthamini wa madini ya almas  TANSORT  kwa kufanikisha ushiriki wetu lakini bado naiomba Serikali  iendelee kutoa mafunzo mbalimbali kwa wachimbaji na wafanyabiashara wa madini”.  Aliongeza Jeremiah.
Akizungumzia ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo, Kamishna Msaidizi wa Madini, Mhandisi Hamis Komba, alieleza kuwa, Serikali ina mengi iliyojifunza kutokana na ushiriki wake katika maonesho hayo ikiwemo matumizi ya  teknolojia zinazotumika katika sekta hiyo.
Aliongeza kuwa, watanzania wakiwemo wafanyabiashara na wachimbaji wanatakiwa kuwa na uthubutu ili waweze kuleta mapinduzi na mabadiliko katika sekta hiyo, hali ambayo  itawasaidia kuendana  na biashara za nje  ikiwemo pia ushindani wa kimataifa.
Aidha, alieleza kuwa, uwezo wa kuibadilisha Tanzania kupitia sekta ya madini upo hivyo, amewataka wadau wote kila mmoja atekeleze wajibu wake kikamilifu.
“Tunatakiwa kujipanga, kwa mfano kwenye usonara kuna mengi, tunahitaji kuufikisha usonara katika ngazi za kimataifa kuanzia teknolojia. Kila mdau analo jukumu, wafanyabiashara na wachimbaji kuweni na uthubutu, wataalamu nyanyukeni muisaidie Serikali”.  Amesema Komba.
Akizungumzia kuhusu uthamini wa madini ya vito na almas katika maonesho hayo, mthamini wa madini kutoka idara ya uthamini  wa madini ya almas TANSORT Bw. Edward Rweymamu alieleza kuwa, idara ya uthamini imeyatumia maonesho hayo kutafiti mwenendo wa bei za madini jambo ambalo litawasaidia kuifanyia marekebisho   kanzidata  ya bei ili kuhakikisha wanapata mrahaba stahiki.
Ameongeza kuwa, si kwa wafanyabiashara na wachimbaji pekee ambao wamenufaika na maonesho hayo bali hata nchi ya Tanzania kutokana na idadi kubwa ya wageni waliotembelea banda la Tanzania kutafuta madini mbalimbali yakiwemo madini ya Tanzanite, Ruby, Saphire na Almas, yakiwemo pia madini ya viwandani hali ambayo inaashiria kukubalika kwa madini ya Tanzania katika soko la Kimataifa.
Katika hatua nyingine, wafanyabiashara na wachimbaji waliipongeza Serikali na Wizara ya Nishati na Madini kupitia Kitengo cha Uthamini wa madini ya Almas (TANSORT)  kwa kuratibu na kufanikisha ushiriki wa Tanzania kwa mara ya kwanza katika maonesho hayo ambayo yamewasaidia kufungua mipaka ya kibiashara.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top