Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI WA MAJI JUMANNE MAGHEMBE AZINDUA MAADHIMISHO YA 26 YA WIKI YA MAJI KITAIFA

 Waziri wa Maji Profesa.Jumanne Maghembe (katikati), akikata utepe kuzindua rasmi maadhimisho ya 26 ya wiki ya maji yanayofanyika kitaifa katika uwanja wa jamuhuri Mkoani Dodoma Machi 16-22,2014 (kushoto), Katibu Mkuu wa wizara hiyo  Enjinia Bashir  Mrindoko, na kulia Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt.Rehema Nchimbi.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt.Rehema Nchimbi akiongea  kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, kuhusiana na maendeleo ya miundo mbinu ya maji  kupitia mpango wa matokeo  makubwa sasa.
  Waziri wa Maji Profesa.Jumanne Maghembe akisoma hotuba yake Machi 16, 2014 wakati akizindua rasmi maadhimisho ya 26 ya wiki ya maji yanayofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamuhuri Mkoani Dodoma,mara baada ya kufanya uzinduzi huo Waziri Maghembe, amewataka wananchi kuacha kutumia kuni na mkaa kwa matumizi ya nyumbani  na badala yake kutumia gesi kama nishati mbadala Maadhimisho hayo yanayolenga kuelimisha jamii juu ya matumizi bora ya maji na mazingira , huku kauli mbiu ikiwa ni Uhakika wa Maji na Nishart.
 Baadhi ya viongozi wa serikali pamoja wananchi  wakishuhudia uzinduzi huo.
  Kikundi cha ngoma cha asili ya Kigogo kikitoa burudani kwenye maadhimisho ya 26 ya wiki ya maji yanayofanyika kitaifa mkoani Dodoma.
 Kikundi cha ngoma cha JKT kikitoa burudani.
 Mhandisi Uendeshaji kutoka DUASA, Luchanganya Nkonogumo akimuelezea Waziri wa Maji Profesa.Jumanne Maghembe kuhusiana na kifaa cha kisasa kwajili ya kipimia mifereji ya maji.
 Mhandisi Mkuu Wizara ya Maji, Mwanaidi Muyimondi akimunyesha Waziri wa Maji Profesa.Jumanne Maghembe takwimu wa ufatiliaji wa maji vijijini.baada ya kutembelea banda la Wizara ya Maji.
 Meneja Masoko wa Kapuni ya Pipes Industries Ezra Chiwelesa akimuelezea Waziri wa Maji Profesa.Jumanne Maghembe kuhusiana pampu za kusafirishia maji pamoja na ufanyaji kazi wake.
Waziri wa Maji Jumanne Maghembe akisalimiana na wanafunzi wa shule mbalimbali mara baada ya kuzinua maadhimisho hao.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top