Katibu
Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Sasi Salula akikagua moja ya miradi
katika wilaya mpanda inayotekelezwa na program ya uhifadhi wa ziwa
Tanganyika., hapo ni mradi wa maji ulioko kijiji cha Isengule kata ya
IKola.
…………………………………………….
Na Kibada Kibada -katavi
Katibu
Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Sasi Salula amefanya ziara ya
kutembelea miradi inayofadhiliwa na ofisi yake katika ukanda wa Ziwa
Tanganyika Wilayani Mpanda Mkoani Katavi na kujionea hali halisi ya
miradi inavyoendelea kutekelezwa na kagiza kukamilika mapema
iwezekanavyo.
Agizo
hilo amelitoa baada ya kukuta baadhi ya miradi ikiwa katika hali
isiyoridhisha na kupata hofu kama inaweza kukamilika kwa wakati ili
kwenda sawasawa na mkataba na wafadhili, hivyo akaagiza zichukuliwe
hatua za haraka kukamilisha miradi hiyo kabla ya muda kuisha.
Miradi
hiyo inasimamiwa na program ya uendelezaji na Uhifadhi mazingira wa
Bonde la ziwa Tanganyika katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi , na
makao makuu ya miradi hiyo iko mkoani kigoma na ofisi ya makamu wa Rais
ndiyo inayosimamia .
Amesema
watu wanaoishi Nchi zinazozungukwa na ziwa Tanganyika wanakaribia
karibu milioni kumi, na wanakabiliwa na changamoto ya uharibifu wa
mazingira, hivyo hatua za makusudi zisipochukuliwa kuhakikisha
mazingira ya ziwa hilo yanahifadhiwa huenda uchumi wa wananchi hao hasa
wale wanaotegemea ziwa Tanganyika ukawa mashakani.
Aliitaja
miradi ya inayotekelezwa kwa upande wa mkoa wa Katavi Katika wilaya ya
Mpanda , ukanda wa Ziwa Tanganyika kuwa ni miradi ya Elimu , Afya,
Maji na Ujenzi wa Mwalo unaojengwa kwenye kijiji cha Ikola Kata ya Ikola
kwa thamani ya shilingi milioni 800, fedha zilizotolewa na wafadhili
kwa ajili ya kuwaletea Maendeleo wananchi wanaozunguka ukanda huo.
Akiwa
katika Kijiji cha Ikola kukagua ujenzi wa Mwalo ameitaka Halmashauri
kusisimamia ujenzi wa mwalo huo na kukamilika mara moja kabla ya muda
uliopangwa na wafadhili kumalizika.
Mkandarasi
anayejenga mwalo ameshalipwa kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili
ya kazi iliyofanyika hadi hapo ilipofikia ikiwa ni pamoja na ujenzi wa
soko la kuuuzia samaki, na maeneo mengine muhim
Post a Comment