Mtu mmoja
anaesadikiwa kuwa ni jambazi ambaye hakufahamika jina anayekadiliwa
kuwa na umri wa miaka 25 ameuwawa kwa kupigwa mawe kisha kuchomwa moto
na mwingine kunusurika kuuwawa.
Tukio
hilo limetokea alfajiri ya leo katika kijiji cha Shibula kata ya
Bugongwa wilayani Ilemela Mkoani Mwanza kufuatia tukio la wizi lilotokea
usiku wa kuamkia leo katika mtaa Nyamwilolelwa ambapo pikipiki moja na
paneli ya solar ziliibiwa.Katibu wa Sungusungu katika kijiji cha Shibula
John Mashalia amesema kuwa kufuatia tukio hilo waliamua kuweka ulinzi
shirikishi kuzunguka vijiji vyote na ndipo walipokutana na kijana huyo
aliyeuwawa akiwa na kijana mwingine aliyefahamika kwa jina la Edward
Aloyce ambao walidai wanatafuta pikipiki iliyopotea.
Mashalia
ameongeza kuwa kata ya Bugongwa imekuwa na matukio ya ujambazi mara kwa
mara ikiwa ni pamoja na vitendo vya ubakaji kwa watoto na wanawake.
Kwa
upande wake mkaguzi msaidizi wa jeshi la polisi Joyce Kotecha amewataka
wananchi wa kata hiyo kuacha kujichulia sheria mkononi na kwamba
wawasiliane na uongozi wa kata yanapotokea matatizo ya namna hiyo.
KIJANA ALIYEUWAWA KWA KUCHOMWA MOTO
VIJANA WA SUNGUSUNGU WAKIWA KATIKA MLANGO WA DUKA AMBAPO KIJANA MWINGINE ALIYENUSURIKA ALIFUNGUNGIWA KUNGOJA POLISI
HII NI BODA BODA AMBAYO WALIENDA NAYO ENEO LA TUKIO VIJANA HAO.
POLISI WAKIWASILI ENEO LA TUKIO.
POLISI WAKIPANGA JINSI YA KUMTOA MTUHUMIWA HUYO.
AMBULANCE YA ZIMA MOTO IKIANDALIWA KUPAKIA MAITI YA KIJANA HUYO.
MWILI WA KIJANA HUYO UKIWA CHINI BAADA YA MOTO KUZIMIKA.
POLISI WAKIPAKIA PIKIPIKI ILIYOKUTWA KWENYE TUKIO.
MACHELA IKIANDALIWA KUUPAKIA MWILI HUO.
POLISI WAKIKAGUA MAKOTI AMBAYO KIJANA ALIYENUSURIKA ALIYAVAA.
MWANANCHI NA KILI YA MOTO BAADA YA TUKIO HILO
WANACHI WALIOJITOKEZA KATIKA MWANO HUO
MSAIDIZI WA POLISI INSPECTOR JOYCE KOTECHA AKIWASIHI WANANCHI WATULIE ILI SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE
POLISI WAKIW GETINI KWA MAANDALIZI YA KUMTOA KIJANA ALIYENUSURIKA
MWILI WA KIJANA HUYO UKIPAKIWA KWENYE MACHELA
ASKARI AKIWA STANDBY NA BOMU LA MACHOZI WAKATI WA KUMTOA KIJANA ALIYEFUNGIWA DUKANI
KIJANA ALIYENUSURIKA AITWAYE MANGI AKITOLEWA KUTOKA NDANI YA DUKA KWA ULINZI MKALI NA KUPAKIWA KWENYE GARI
KIJANA AKIWA NDANI YA GARI PEMBENI NI MAITI YA MWENZAKE
KIJANA AKIWA HOI BAADA YA KUPIGWA NAWANANCHI
INASIKITISHA SANA
WAKUU WA USALAMA WAKITOA MAELEKEZO KWA WANANCHI.
VIJANA WA SUNGUSUNGU WAKIWA KATIKA MLANGO WA DUKA AMBAPO KIJANA MWINGINE ALIYENUSURIKA ALIFUNGUNGIWA KUNGOJA POLISI
HII NI BODA BODA AMBAYO WALIENDA NAYO ENEO LA TUKIO VIJANA HAO.
POLISI WAKIWASILI ENEO LA TUKIO.
POLISI WAKIPANGA JINSI YA KUMTOA MTUHUMIWA HUYO.
AMBULANCE YA ZIMA MOTO IKIANDALIWA KUPAKIA MAITI YA KIJANA HUYO.
MWILI WA KIJANA HUYO UKIWA CHINI BAADA YA MOTO KUZIMIKA.
POLISI WAKIPAKIA PIKIPIKI ILIYOKUTWA KWENYE TUKIO.
MACHELA IKIANDALIWA KUUPAKIA MWILI HUO.
POLISI WAKIKAGUA MAKOTI AMBAYO KIJANA ALIYENUSURIKA ALIYAVAA.
MWANANCHI NA KILI YA MOTO BAADA YA TUKIO HILO
WANACHI WALIOJITOKEZA KATIKA MWANO HUO
MSAIDIZI WA POLISI INSPECTOR JOYCE KOTECHA AKIWASIHI WANANCHI WATULIE ILI SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE
POLISI WAKIW GETINI KWA MAANDALIZI YA KUMTOA KIJANA ALIYENUSURIKA
MWILI WA KIJANA HUYO UKIPAKIWA KWENYE MACHELA
ASKARI AKIWA STANDBY NA BOMU LA MACHOZI WAKATI WA KUMTOA KIJANA ALIYEFUNGIWA DUKANI
KIJANA ALIYENUSURIKA AITWAYE MANGI AKITOLEWA KUTOKA NDANI YA DUKA KWA ULINZI MKALI NA KUPAKIWA KWENYE GARI
KIJANA AKIWA NDANI YA GARI PEMBENI NI MAITI YA MWENZAKE
KIJANA AKIWA HOI BAADA YA KUPIGWA NAWANANCHI
INASIKITISHA SANA
WAKUU WA USALAMA WAKITOA MAELEKEZO KWA WANANCHI.
Post a Comment