Timu
ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania iliyotwaa ubingwa wa Dunia wa Watoto
wa Mitaani nchini Brazil baada ya kuifunga Burundi mabao 3-1 kwenye
fainali imetambulishwa leo (Aprili 11 mwaka huu) katika Bunge Maalumu la
Katiba mjini Dodoma.
Baadaye timu hiyo leo itapata
chakula cha mchana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mizengo Pinda. Saa 10 jioni itatembeza kombe hilo katika maeneo
mbalimbali ya Manispaa ya Dodoma katika gari za wazi.
Jioni imeandaliwa hafla maalumu
ya chakula pamoja na burudani hapo hapo mjini Dodoma ambapo mgeni rasmi
atakuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella
Mukangara.
Post a Comment