Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma bango lenye ujumbe wa kulalamikia kodi kubwa wanazotozwa wavuvi wadogowadogo wa Kibirizi,Kigoma.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubianwakazi wa Kibirizi
mkoani Kigoma ambao wanakilio cha kutozwa kodi kubwa, kuvamiwa na
majambazi wakati wa uvuvi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana
na Mama Mawazo Rashid Mawalan mkazi wa Ujiji Kigoma ,Katibu Mkuu
alikuwa akitembea kwenye njia iliyotumika na Watumwa ambapo kuna miembe
yenye umri zaidi ya miaka 150.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mzee Masoud Mwinyi
Chande kwenye mnara wa kumbukumbu ya nyumba ya kwanza ambayo Mwalimu
Julius Nyerere alifikia Ujiji wakati akifanya harakati za kutafuta
Uhuru, Nyumba hiyo inasemekana Mwalimu Nyerere alifika akiongozana na
Suleiman Takadili na Bibi Titi Mohamed.
Post a Comment