Wasichana ambao kundi la Boko Haram liliwateka nyaraKiongozi
wa kundi la Boko Haram Abubakar Shekahu amesema kuwa atawaachilia huru
wasichana waliotekwa nyara iwapo tu wapiganaji wa kundi hilo
wanaozuiliwa na serikali ya Nigeria wataachiliwa huru.
Katika
kanda mpya iliyotolewa na kundi hilo, kiongozi huyo, amesema kuwa
wasichana hao waliweza kusilimu katika kipindi cha wiki nne zilizopita
tangu watekwe nyara.
Kanda
hiyo inaonyesha zaidi ya wanawake miamoja wakiwa wamevalia hijabu na
kuswali. Abubaka Shekau anasema kuwa wanawake hao ni wasichana
waliotekwa nyara na kundi hilo.
Walitekwa nyara kutoka katika shule yao mjini Chibok, Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo
Rais wa Ufaransa amejitolea kuwa mwenyeji wa mkutano utakaotafuta njia za kupambana na Boko Haram.
chanzo bbc swahili
Post a Comment