Vicky Kamata akiwa katika pozi na mwanaume aliyepanga kuoana naye anayejulikana kwa jina la Charles wa jijini Dar.
KATEKISTA AZUNGUMZA NA IJUMAA WIKIENDA
Hadi
gazeti hili linaondoka kwenye Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria
Mama wa Mkombozi, Sinza jijini Dar juzi saa 10:00 jioni, ndoa ya Mbunge
Vicky Kamata iliyokuwa ifungwe hapo iliyeyuka.
Vicky
Kamata ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya UVCCM, Mkoa wa
Geita alikuwa afunge ndoa na mwanaume aliyejulikana kwa jina la Charles
wa jijini Dar.Baada ya kuona muda unakwenda bila kuwepo kwa
dalili za wahusika kufika kufunga ndoa hiyo ambayo harusi yake ilidaiwa
ingetumia shilingi milioni 96, wanahabari wetu walimtafuta Baba Paroko,
Cuthbert Maganga ili kumsikia anasema nini kuhusu hilo.Hata hivyo, mtu aliyedai ni katekista wa kanisa hilo alisema paroko alikwenda hija, Buguruni, Dar.
Kuhusu ndoa ya Vicky Kamata, katekista huyo alidai Jumapili ya Mei 18, 2014 ndani ya ibada za kanisa hilo ilitangazwa hadharani ‘laivu’ kwamba haitafungwa.


Post a Comment