WASANII wawili
wa filamu, Nice Mohamed ‘Mtunisi’ na Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ambao
walikuwa wapenzi kabla ya kuachana na mwanaume huyo kuoa, sasa
wamerudiana rasmi.
Kwa
mujibu wa chanzo chetu kilicho jirani na wasanii hao kimesema wawili
hao hivi sasa wanapika na kupakua.Kilisema baada ya kurudiana, kwa sasa
wanaishi pamoja kama mume na mke maeneo ya Sinza, jijini Dar es Salaam
huku wakiishi kwa amani na upendo.
kilisema chanzo hicho.
Hivi karibuni Batuli aliweka picha ya Mtunisi katika akaunti yake kwenye mtandao wa Instagram na kuandika maneno haya
Hivi karibuni Batuli aliweka picha ya Mtunisi katika akaunti yake kwenye mtandao wa Instagram na kuandika maneno haya
Alipotakiwa
kuzungumzia suala hilo, Batuli alisema hawezi kuzungumzia katika vyombo
vya habari kwa vile mambo hayo ni maisha yake binafsi.
Kwa
upande wake, Mtunisi alicheka na kudai kusikia kutoka kwa watu juu ya
mwenzake kuweka picha yake mtandaoni na kuandika maneno ya kimahaba,
kitu alichosema hawezi kuzuia nafsi ya mtu kumuweka moyoni.
Post a Comment