Kesi iliyofunguliwa na baadhi ya wanachama wa klabu ya Simba kuhusu
kuzuia kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa timu hiyo imeahirishwa leo
na jaji wa Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
Wanachama hao walifungua kesi hiyo baada ya Michael Wambura kuondolewa katika kinyang’anyiro cha uchaguzi.
Tovuti hii ilifika katika viwanja vya Mahakani Kuu Dar es Salaam na
kukuta wanachama hao wakiondoka huku wakilalamika njiani kuwa kesi hiyo
inapigwa danadana mpaka Mwenyekiti Ismail Rage akifike mahakamani hapo.
Kwa mujibu wa wanachama hao kesi hiyo itasikilizwa kesho atakapofika
Rage, lakini huku wagombea wa nafasi mbalimbali wakiendelea na kampeni
za uchaguzi, ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 29 mwezi huu.
>>>Taarifa News
Post a Comment