Luke Shaw amekamilisha dili la usajili la paundi milioni 31.5 katika klabu ya Manchester United.
BEKI
wa kushoto wa England, Luke Shaw amekamilisha usajili katika klabu ya
Manchester United kwa dau la paundi milioni 31.5 na kusaini mkataba wa
miaka minne kukipiga Old Trafford.
Nyota
huyo kinda amefuzu vipimo vya afya leo katika uwanja wa mazoezi wa
Carrington na imetaarifiwa kuwa atakuwa chaguo la kwanza la kocha Louis
van Gaal katika nafasi ya kushoto.
Inafahamika
kuwa kinda huyo atahakikishiwa nafasi ya kuanza, huku beki mkongwe
mwenye miaka 33, Mfaransa, Patrice Evra ambaye atabakia kwa mwaka mmoja
akipunguziwa majukumu.
Historia: Shaw alisema amejisikia furaha kujiunga na mabingwa mara 13 wa ligi kuu ya England
Shaw ameelezea furaha yake ya kujiunga Man United kwenye mtandao wa Twita
Shaw amekaribishwa pia na Wayne Rooney
Mchezaji
huyo wa zamani wa Southampton amesaini mkataba wa miaka minne huku
kukiwa na kipengele cha kuongezewa mwaka mmoja zaidi na amefurahi sana
kujiunga na mashetani hao wekundu.
Post a Comment