Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MATESO MAKALI ; ANGALIA MWANAFUNZI HUYU ANAVYOTESEKA, MSAADA WAKO UNAHITAJIKA

Kijana Amos Ng’arare Sasi mwenye umri wa miaka 21, mkazi wa Kijiji cha Kizaru, Kata ya Mryaza, Musoma vijijni anyesumbuliwa na uvimbe.
Kwa karibu miaka 17 sasa, kijana Amos Ng’arare Sasi mwenye umri wa miaka 21, mkazi wa Kijiji cha Kizaru, Kata ya Mryaza, Musoma vijijni anataabika kwa ugonjwa ambao umempeleka katika hospitali nyingi bila mafanikio.
 Kama angeendelea na masomo yake vizuri, hivi sasa Amosi angekuwa kidato cha nne, lakini alilazimika kukaa nyumbani na kuwaacha wenzake wakiendelea na masomo katika Shule ya Sekondari ya Bumangi kutokana na uvimbe kuzidi kukua.
 Kwa sasa yupo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili anakotibiwa. Akizungumza na mwandishi wa habari hii alikuwa na mengi ya kusimulia:
 “Ninaumia sana moyoni niwaonapo wanafunzi wenzangu niliosoma nao darasa moja wakiendelea na masomo wakati miye nakabiliana na gonjwa hili la ajabu ambalo limezima ndoto zangu juu ya elimu, sitegemei kurudi tena darasani, nilizaliwa nikiwa sina tatizo kiafya, nililelewa na wazazi wangu wote wawili, nikawa naishi vizuri kama watoto wenzangu.
Kijana Amos Ng’arare Sasi akiendelea kuugua kwa uvimbe katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
 “Tatizo lilianza kama kaupele hivi nikiwa na umri wa miaka minne, kidogo kidogo kikawa kinakua, lakini bahati mbaya baba alifariki na mama akabeba mzigo wa kunihudumia kwa matibabu, licha ya kipato chake kidogo kwani alitegemea kilimo, tena cha jembe la mkono.
 “Pamoja na mama kunipeleka hospitali mbalimbali, nilikuwa napewa asprini tu kwa ajili ya kutuliza maumivu kwani walishindwa kunipa dawa za aina nyingine kutokana na ugonjwa wangu kutofahamika.
 “Mama anahangaika na mimi hadi namuonea huruma, kaka yangu mkubwa alitoweka nyumbani tangu mwaka 1998 akisema anaenda kutafuta kazi, mpaka sasa hajulikani alipo na wala hajawahi kurudi nyumbani, hali ilizidi kuwa mbaya nilipofikisha umri wa miaka tisa, maumivu na uvimbe ukazidi.
 “Mama alikuwa hapati usingizi aliponiona nahangaika, alinipeleka hospitali ya Musoma haikusaidia, mwaka 2010 nilipelekwa Bugando kufanyiwa uchunguzi, ugonjwa haukujulikana, wakati huo ndiyo nilikuwa nikianza kidato cha kwanza, nilienda siku chache.
 “Nilirudishwa nyumbani, baadhi ya watu wakawa hawataki kuniona mitaani, wakaniona kama vile nimeleta nuksi katika ukoo, nikawa najificha ndani.
 “Baadhi ya wananchi walinionea huruma walinichangishia fedha ili nije Muhimbili, mara ya kwanza nilifika hapa Septemba 2011, nikachukuliwa vipimo na kuambiwa nirudi nyumbani hadi Desemba.
“Hata hivyo, sikuweza kurudi kipindi hicho kutokana na kukosa nauli, baadaye nikafanikiwa kwenda nyumbani. Tatizo likawa namna ya kufuata majibu, lakini baadaye nilipata.
 “Mara ya pili nilikuja Februari mwaka huu kwa msaada wa nauli kutoka kwa diwani wetu pamoja na Mbunge Nimrodi Mkono, walinipima kwa mara ya pili na kunieleza kuwa kuna mshipa wa fahamu unapitisha damu nyingi hivyo natakiwa kufanyiwa upasuaji nchini India.
 “Kuna kipindi napata maumivu hadi napoteza fahamu, uvimbe unazidi kufunika macho, sioni vizuri, madaktari wapo karibu na mimi, wananipa dawa za kupunguza maumivu, wananisaidia sana, ninawashukuru, lakini naumia zaidi ninapowaona wagonjwa wenzangu wakitembelewa na ndugu zao, mimi sina mtu hata mmoja.
 “Ninaomba Watanzania wenzangu wanisaidie, japo kwa maombi ili niweze kupata msaada wa kwenda India kwa matibabu, napenda nipone, nirudi nyumbani kumuona mama.” 
Kwa walioguswa na simulizi ya kusikitisha ya Amos wanaweza kumsaidia ushauri au fedha kupitia simu zake za kiganjani ambazo ni 0765 765747 na 0715 756384.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top