Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MIKUTANO YA NAPE NNAUYE YAPIGWA MARUFUKU MTWARA, MWENYEWE ADAI HUO NI UBAKAJI WA DEMOKRASIA

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye ameonja chungu ya uamuzi wa Serikali wa kusitisha mikutano ya hadhara katika mikoa ya Lindi na Mtwara baada ya kushindwa kufungua mashina ya chama hicho mjini Mtwara. 
 
Nape ambaye alikuwa mkoani Mtwara kwa ziara ya siku moja, alijikuta akiishia kuwakabidhi bendera za chama hicho viongozi wa matawi ili wakazipandishe wenyewe kimyakimya.
 
Akizungumzia hatua hiyo, Nape alisema amri hiyo ya kusitisha mikutano imekuwa kikwazo na inadidimiza demokrasia katika mikoa hiyo, hivyo Serikali inapaswa kuibadili ili kuruhusu iendelee kufanyika. Mashina ya chama hicho ambayo yalitarajiwa kufunguliwa mwishoni mwa wiki ni Shapriya, Coco Beach na Kwajionee.
 
“Ni kweli ilikuwa twende kuzindua kwenye maeneo yenu lakini… lipo agizo ambalo lilitolewa na Serikali kuzuia mikutano katika mikoa hii, kupitia kwenu ipo haja ya kufungua mikutano ili demokrasia ipanuke zaidi,” alisema Nape na kuongeza:
 
“Amri hii kwa mtazamo wangu inabaka demokrasia, lazima mikutano iruhusiwe kama hali ni mbaya, kazi ya Serikali ni kulinda huo usalama… nitakwenda kushauriana nao ili mikutano ifunguliwe, sidhani kama masikio yanaweza kuzidi kichwa.”
 
Akizungumzia hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Maisha Maganga alisema Serikali haijatengua agizo hilo.
Credit:  Mwananchi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top