Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI PROF. MUHONGO ABANWA BUNGENI

 

Kufuatia umeme kukatika ndani ya bunge wakati wa kupiga kura za kupitisha bajeti kuu ya serikali 2014/2015, hali hiyo imelikwaza bunge na kulazimu spika Anna Makinda kumtaka waziri wa nishati na madini kueleza sababu za tatizo hilo. 
Akizungumzia suala hilo bungeni Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo ameanza kwa kuomba radhi na kudai kuwa umeme haukukatika bungeni pekee bali umekatika nchi nzima.
 Prof Muhongo amesema  sababu ya kukatika umeme ni mitambo ya kufua umeme inayotumia maji, mafuta na gesi imechoka ghafla na kwa mpigo hali iliyosababisha umeme kukatika kwa zaidi ya nusu saa. 
Aidha waziri huyo ameiagiza Tanesco kuomba radhi watanzania kwa tatizo hilo na kutoa maelezo ya kitaalamu ya kwa nini umeme umekatika nchi nzima haraka iwezekanavyo. 
Kukatika huko kwa umeme hii leo kumepelekea kukwama kwa zoezi la kupiga kura bungeni ili kupitisha bajeti kuu ya serikali.
hata hivyo zoezi la kupiga kura limekamilika baada ya umeme kurudi ambapo wabunge 300 wamepiga kura, kati yao 234 wamesema ndiyo bajeti ipite na 66 wamesema hapana isipite, hivyo bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2014/2015 kupitishwa. 
Na Edwin Moshi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top