Kizungumkuti
cha usajili barani Ulaya kimeanza kushika kasi huku timu zikijiandaa
kwa ajili ya msimu mpya wa soka barani ulaya.Miezi kadhaa iliyopita
klabu ya soka ya Chelsea ilithibitisha rasmi kwamba haitomuongezea
mkataba mpya mchezaji Ashley Cole ambaye alijiunga na timu hiyo mwaka
2003 akitokea Arsenal. Baada ya taarifa hiyo timu nyingi zikaanza
kuhusishwa na usajili wa mchezaji huyo.Leo hii imethibitishwa rasmi
kwamba mchezaji huyo amejiunga rasmi na timu ya AS Roma ya Italia.
Cole
ambaye alikuwa akilipwa mshahara wa Paundi 185,000 kwa wiki na Chelsea
imekubali kupata kiasi cha £160k kwa makubaliano ya kulipwa kiasi
kisichozidi £35,000 kwa wiki na klabu hiyo ya Serie A.
Ashley Cole amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu hiyo ya Rome.
Post a Comment