Zaidi
ya Maofisa kutoka wizara tatu wapato 13 waliokuwa wakifanya kazi katika
uwanja wa kimataifa wa Ndege wa Mwl. Julius Nyerere, wamerudishwa
katika wizara zao kwa kosa la kupokea rushwa kwa wageni wanaoingia
kutoka nchi mbalimbali.Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es
Salaam Waziri wa Uchukuzi Dr. Herrison Mwakyembe alisema kuwa, maofisa
hao walikuwa katika kitego cha Wizara ya Kilimo, Wizara ya Afya na
Wizara ya Mifugo na Uvuvi.Wageni ambao walikuwa wanakaguliwa na kuobwa
rushwa na wafanyakazi hao ni kutoka nchini China, India na Nchi za
Kiarabu, ambao wakifika uwanjani hapo wanakaguliwa mabegi kama amebeba
dawa za asili dawa hizo huchukuliwa na maofisa wa kilimo na baadae
kuobwa pesa na kurudishiwa dawa hizo.
Pia
kama ameingia hajachoma sindano ya homa ya manjano anaamriwa na
kuulizwa kwanini hujachoma na akioneakana anakaidi anaambiwa atowe
chochote kitu kisha anaachiwa, hivyo hivyo kwa upande wa uvuvi na mifugo
nako wanafanyiwa hivyo.
Kufuatia
malalamiko hayo ya wageni wanaoingia hapa nchini, wageni hao waliamua
kuyapeleka kwa Waziri Mwakyembe, naye bila ya kusita aliunda tume ambayo
iliangalia kamera za usalama na kupata maofisa 13 waliobainika kufanya
uchafu huo, ambao unachafua taswira ya nchi yetu na kuwakimbiza
wawekezaji
Post a Comment