BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
HIGHER EDUCATION STUDENTS’ LOANS BOARD
Plot No. 8, Block No. 46, Sam Nujoma Road, Mwenge; P.O. Box 76068, Dar es Salaam, Tanzania
Tel: (General) +255 22 2772432/2772433; Fax: +255 22 2700286; E-mail: info@heslb.go.tz Website:www.heslb.go.tz
Bodi
ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kuwatahadharisha
waombaji wa mikopo na umma kwa ujumla, juu ya kuibuka kwa genge la
matapeli wanaowalaghai wananchi ambapo hujitambulisha kuwa wao ni
wafanyakazi wa Bodi ya Mikopo.Mbinu
zinazotumiwa na genge hilo la matapeli ni kuwatumia ujumbe mfupi wa
simu waombaji wa mikopo ukiwatahadharisha kuwa fomu zao za maombi ya
mikopo zina dosari na hivyo wanatakiwa watume sh. 15,000.00 kwa kutumia
utaratibu wa kutuma Fedha kwa njia ya mitandao ya simu kwenda kwenye
namba za simu za matapeli hao ili fomu zao za mikopo ziweze kufikiriwa. Katika
utapeli huo, matapeli hao wanawatishia waombaji wa Mikopo wanaoendelea
na masomo kuwa wasipohuisha taarifa zao za kuendelea kupokea Mikopo
mwaka ujao wa kitaaluma 2014/2015 hawatapata Mikopo.
Bodi ya Mikopo inapenda kuwafahamisha waombaji wa Mikopo na umma kwa ujumla kwamba:
(i)
Waombaji mikopo wanatakiwa kutuma fomu zao au taarifa zilizokosekana
kwa njia ya Posta tu. Bodi haijaweka wakala mwingine yeyote anayetoza
ada kwa ajili hiyo.
(ii)
Ada zote za maombi ya mikopo zilielekezwa kulipwa kwa njia ya M-Pesa
kwa utaratibu ambao umeelekezwa bayana kwenye ukurasa wa maombi kwa njia
ya mtandao (http://olas.heslb.go.tz) na si vinginevyo.
(iii)
Waombaji wa Mikopo wanaoendelea na masomo hawatakiwi kujaza fomu za
maombi ya Mikopo kama ilivyokwisha kufafanuliwa katika Mwongozo wa
Utoaji Mikopo kwa mwaka wa masomo 2014/2015.
(iv)
Waombaji mikopo watakaopokea simu au ujumbe mfupi wa simu unaowataka
watume Fedha ili wapatiwe huduma ya kuhuisha taarifa zao za mkopo watoe
taarifa kuhusu matapeli hao kwa Polisi au TAKUKURU kusudi hatua za
kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya wahalifu hao.
IMETOLEWA NA:
KAIMU MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Post a Comment