Kwa
wasikilizaji wengi wa kipindi cha XXL cha Clouds FM, July 2 itabaki
kwenye kumbukumbu zao baada ya kusikia kitu kisicho cha kawaida na
ambacho hakijawahi kutokea tangu redio za FM zije Tanzania.
Apparently,
watangazaji hao akiwemo B12, Adam Mchomvu na DJ Fetty walikuwa
wanabishana kuhusu jambo fulani lililowafanya wapoteze uvumilivu na
kuanza kushikana na kisha kurushiana makonde.
Kwenye kipande hicho cha sauti vinasikika vitu mbalimbali zikiwemo mic za studio vikikurupushwa.
Post a Comment