Ndege Mnana, Linah ambaye kwa muda mrefu amekuwa kimya bila kuachia wimbo mpya kabla ya kuachia remix ya wimbo wa Kizaizai wa Diamond ameeleza sababu zinazomfanya aendelee kuishi maisha mazuri hata anapokuwa hana wimbo mpya redioni kiasi cha kupunguza mfululizo wa shows.
Linah alifunguka katika Power Jams ya East Africa Radio jana kuwa
sababu kubwa inayomfanya aendelee kung’aa mjini hata bila shows wala
kuwa na nyimbo mpya ni kujipanga mapema kuikabili hali yoyote
itakayojitokeza kwenye maisha yake kama mwanamuziki.
“Labda niseme kitu kimoja, unajua unapokuwa msanii unatakiwa ujipange
vya kutosha. Anything can happen. Kwa hiyo unapofanya kazi at the time
unapokuwa vizuri inabidi ujipange kwa maisha ya mbele pia. Kama mimi
nilikuwa nimejipanga enough kwamba in case ikitokea kitu chochote mimi
niko sawa. Yaani sitatetereka.”
Amesema anajua msanii anapotetereka anamuangusha shabiki wake anapotaka kujigamba kwa wenzake jinsi anavyomkubali msanii huyo.
Post a Comment