Kumbe! Sexy
lady wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kwamba
amewajua wabaya wake wanaomfuatilia na kumsakama kwa ubaya katika maisha
yake, amewaonya kuwa dawa yao ipo jikoni.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda
wikiendi iliyopita jijini Dar, Lulu alisema kuwa kila kukicha lazima
watu hao waibuke na jipya linalomhusu yeye, mbaya zaidi ni kwa ajili ya
kumchafua.
“Mara utasikia Lulu kagombania bwana,
mara Lulu kafanya sijui kitu gani lakini ukiangalia hakuna hata cha
ukweli kwa kuwa nimekuwa staa basi kila mtu ana lake la kuongea, kifupi
nimeshawajua wabaya wangu na kwamba ni wengi sana, nawaambia niko njiani
kuwaandalia dawa yao ambayo naamini itakuja kuwa fundisho kwao na kwa
wengine,” alisema Lulu.
Hii ni mara ya kwanza kwa muigizaji
huyo kufunguka kuhusu suala hilo lakini Ijumaa Wikienda linamuomba
asichukue sheria mkononi kwani kibao kinaweza kumgeukia.
Post a Comment