Stori: Musa Mateja
MOYO unauma!
Staa wa R&B Bongo, Juma Khalid ‘Jux Vuitton’ amekiri kuteswa na
ishu ya mwanamitindo Jacqueline Fitzpatric Cliff ‘Jack Patrick’ akiomba
asiulizwe habari za modo huyo aliyekuwa mpenzi wake ambaye kwa sasa yupo
nyuma ya nondo kwa madai ya kukamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’ huko
Macau, Hong Kong nchini China.
Staa wa R&B Bongo, Juma Khalid ‘Jux Vuitton’
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, jamaa huyo alisema kuwa kwa sasa
hapendi kabisa kusikia mtu akimuuliza habari zinazohusiana na mpenzi
wake huyo, kwani zinamtoa kwenye ‘mudi’ na badala yake ana mambo mengi
ya kuzungumza.
‘Jux Vuitton’ akiwa na Jack Patrick.
“Naomba mtu asiniulize ishu za Jack, zinanitibua na zimeshazungumzwa
sana hivyo sioni kipya cha kuzungumzia zaidi ya muziki wangu, kwa sasa
nina projekti mpya kibao zinakuja,” alisema Jux anayetamba na ngoma ya
Nitasubiri aliyomuimbia Jack.
Post a Comment