Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MIROSLAV KLOSE AVUNJA REKODI NA KUWA MFALME WA MABAO KOMBE LA DUNIA, AMTINDUA GWIJI WA BRAZIL RONALDO

      

                    
Record breaker: Miroslav Klose is the top scorer in World Cup history
Mvunja rekodi: Miroslav Klose ni mfungaji bora katika historia ya kombe la dunia.
Miroslav Klose amevunja rekodi ya Ronaldo na kuwa mfungaji mwenye mabao mengi zaidi katika historia ya fainali za kombe la dunia.
Mshambuliaji huyo wa Ujerumani alifunga bao la pili katika ushindi wa mabao 7-1 dhidi ya Brazil kwenye mchezo wa nusu fainali wa kombe la dunia na kufikisha mabao 16.
Lilikuwa bao lake la pili katika mashindano baada ya kufunga bao akitokea benchi katika mchezo dhidi ya Ghana,  hatua ya makundi na kumfanya alingane mabao na gwiji wa Brazil.
Historic: The strike that made hm the record holder
Historia: Shuti lililomfanya ashikilie rekodi ya dunia
 
 WAFUNGAJI  WA JUU WALIOVUNJA REKODI :
Miroslav Klose 16 goals
Ronaldo 15
Gerd Muller 14
Just Fontaine 13
Pele 12
Jurgen Klinsmann 11
Gary Lineker 10
Klose alicheza kwa mara ya kwanza fainali za kombe la dunia mwaka 2002 na kufunga mabao matatu `hat-trick` katika ushindi wa mabao 8-0 dhidi ya  Saudi Arabia. 
Alifunga tena bao katika mechi iliyofuata ya makundi ambayo Ujerumani ilitoka sare ya 1-1 dhidi ya Jamhuri ya  Ireland, kabla ya kufunga bao la pili katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Cameroon.
Licha ya Ujerumani kufika fainali mwaka ule, Klose alishindwa kufunga tena katika mashindano, akimaliza michuano kwa idadi sawa ya mabao na Rivaldo, nyuma ya mfungaji bora, Ronaldo aliyefunga mabao 8.
Miaka minne baadaye, Ujerumani walikuwa wenyeji wa fainali za dunia (2006), mshambuliaji huyo alifunga mabao matano tena ambayo yalitosha kumpatia kiatu cha dhahabu.
Finisher: The German forward scored his 15th goal in finals in the 2-2 draw with Ghana
Nodder: Klose peels away after scoring against Cameroon during the 2002 World Cup
Nutter: The forward leaping to head the equaliser against Argentina in the 2006 quarter-final
Slipped in: Klose scoring the opener of a 4-1 victory against England in the last-16 in 2010
Alifunga mabao mawili katika mchezo wa ufunguzi dhidi ya Costa Rica ambao walishinda mabao 4-2, alifunga mengine mawili katika mchezo wao wa mwisho wa makundi dhidi ya Ecuador.
Klose bao lake la mwisho katika fainali za kombe la dunia mwaka huu lilikuwa katika dakika ya 80. Bao la kusawazisha dhidi ya Argentina kwenye mchezo wa robo fainali na kufanya matokeo yawe 1-1, na Ujerumani wakashinda kwa mikwaju ya penati.
Na mwaka 2010, alifanikiwa kufunga mabao mengine manne: moja kwenye mchezo wa ufunguzi dhidi ya Australia, lingine katika ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya England hatua ya makundi na mawili katika ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Argentina hatua ya robo fainali.
        
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top