Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MKUU WA MKOA WA NJOMBE AKABIDHIWA VYANDARUA 31,000 KWA AJILI YA HOSPITALI NA VITUO VYA AFYA VYA MKOA HUO

 





 Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi

 
 Dr. Leonard Maboko Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii ya TAG ambae pia ni Mkurugenzi wa NIMR, akitoa neno kwa wageni

Na James Festo, Njombe.

MKUU wa Mkoa wa Njombe Capten Mstaafu Assery Msangi, amezitaka taasisi mbalimbali za kijamii na za kidini Nchini kuendelea kusiadia serikali katika kutatua changamoto mbalimbali kwa wananchi ikiwemo sekta ya afya.

Ameyasema hayo mara baada ya kukabidhiwa vyandarua 3100 vinavyotarajiwa kusambazwa kwenye  hospitali 11 pamoja na vituo vya Afya 25 vilivyopo  katika Mkoa wa Njombe kutoka kanisa la Tanzania Assemblies of God  ambalo linaendelea kutoa misaada hiyo ikiwa ni sehemu ya kuelekea maadhimisho  ya  jubilii ya miaka 75 tangu kuanzishwa  kwake.


Wakati huo huo Msangi aliwataka viongozi wa kidini nchini kuendelea kuliombea taifa katika msimu huu wa mchakato wa kuipata katiba mpya , sambamba na uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika  hivi karibuni  pamoja na uchaguzi mkuu wa mwakani.

Kwa upande wake askofu wa kanisa la T. A. G  Njombe,  Patrick Saimon  Luhwango  akisoma taarifa  ya ugawaji wa vyandarua hivyo alisema kuwa mkoa wa Njombe umepewa vyandarua hiyvo kwa lengo la kuwakinga na ugonjwa wa maralia.

Alisema kuwa idadi ya vyandarua ambavyo vimegawiwa kwa mikoa mitatu ya  Njombe, Rukwa Mbeya inatokana na upembuzi yakinifu uliofanywa na wataalamu kutoka kanisa hilo kwa kushirikiana na waganga wa hospitali za wilaya za mikoa hiyo ambapo   uliobaini kuwepo kwa uchache wa vyandarua hivyo.

Thomas Lujuo ni kaimu mganga mkuu wa Mkoa wa Njombe alikiri kuwepo kwa uchache wa vitendea kazi pamoja na vyandarua katika hospitali zilizopo mkoani hapa  hivyo vyandarua vitasaidia kupunguza wagonjwa wapya,  ambapo marelia kwa mwaka jana ili kuwa na asilimia 11 ya magongwa.

"   Msaada huu  wa vyandarua ambao tumeupata  ni muhimu sana kwa sababu kuna maeneo yana idadi kubwa ya wagonjwa wa maralia  hususani katika wilaya ya Ludewa  kwa hiyo kupata masaada huu utatusaidia sana sisi kama mkoa kupunguza vifo vitokanavyo na maralia hasa kwa mama wajawazito"   alisema Mganga huyo.

Katika hatua nyingine Kaimu mganga huyo alibainisha kuwepo kwa  tatizo la utumiaji wa vyandarua kwa wananchi hivyo kuongeza idadi ya  wagonjwa maralia licha ya kuwepo kwa utoaji wa vyandarua bila malipo kupitia mpango wa kudhibiti marelia kwa akina mama wajawazito.

Awali akisoma taarifa hiyo  mbele ya viongozi mbalimbali wa mkoa wa Njombe Askofu Luhwago  alisema kuwa katika jubilii hiyo wanatarajia kugawa vyandarua 8550  kwenye hospitali 34 pamoja na vituo vya afya 83 kutoka mikoa hiyo mitatu na kubainisha kuwa wanatarajia kuhitimisha jubilii hiyo julai 13 mwaka huu  jijini mbeya katika uwanja wa sokoine  ikiwa na kauli mbiu isemayo kuwa"  Mungu anajali roho yako  na mwili wako, jenga mahusiano naye"  huku mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Raisi wa Jamhuli ya Muungano wa Tanzania.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top