MKAZI wa Mbezi Msakuzi, Dar es Salaam, Hassan Ngoso (48), ambaye ni mlinzi wa Shamba, amefariki dunia baada ya kujinyonga.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, alisema tukio hilo lilitokea juzi, saa 10 jioni.
Alisema Ngoso alikutwa amejinyonga huku mwili wake ukiwa unaning’inia
kwenye kamba aliyofunga katika chumba alichokuwa analala.
Kamanda Wambura alisema nyumba hiyo ipo katika shamba linalomilikiwa
na tajiri yake aitwaye Sinyakos Mombeki (45). Sababu za kujinyonga bado
hazijafahamika, na maiti imehifadhiwa Hospitali ya Tumbi.
Katika tukio jingine, mwanamke anayekadiriwa kuwa na umri kati ya
miaka 20 hadi 25, amefariki dunia baada ya kugongwa na gari alipokuwa
anavuka barabara.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Englibert Kiondo, alisema ajali
hiyo ilitokea juzi, saa 8 mchana barabara ya Kilwa, eneo la Kizuiani na
kuhusisha gari T 158 AGD aina ya Scania lenye tela T 198 BMZ. Dereva
wa gari hilo alikimbia baada ya ajali hiyo.
Wakati huo huo, baadhi ya mabanda ya kuhifadhia nguo katika soko la
Ilala, Dar es Salaam, yameteketea kwa moto uliozuka juzi, saa 5 usiku.
Post a Comment