MTOTO mwenye
umri unaokadiriwa kuwa mwaka mmoja ambaye jina lake halikuweza
kufahamika mara moja, aliokotwa huko Kibamba CCM, jijini Dar es Salaam,
nje ya geti la nyumba ya Getruda Gervans.
Tukio hilo lilitokea Juni 24, mwaka huu saa moja na nusu asubuhi huku mfuko wenye nguo zake ukiwa pembeni yake.
Kwa
mujibu wa mama mwenye nyumba hiyo, baada ya kumuokota, alimpeleka Kituo
cha Polisi Mbezi ambako nako walimpeleka katika Hospitali ya
Mwananyamala kabla ya kuhamishiwa Muhimbili.
Afisa
ustawi wa Jamii wodi ya watoto Muhimbili, Grace Julius
alilithibitishia gazeti hili kumpokea mtoto huyo Juni 25, mwaka huu
akitokea Hospitali ya Mwananyamala na akatumia fursa hiyo kulaani tabia
ya kutupa watoto.
Aidha,
aliomba mtu yeyote mwenye taarifa ya kupotea kwa mtoto sehemu yoyote
kufika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo alisema kwa taarifa
zaidi apige simu namba 0788366399.
Mhariri:
Tunakemea vikali vitendo vya unyanyasaji na ukatili dhidi ya watoto na
tunawaomba wananchi kutoa taarifa mara moja kwa mamlaka zinazohusika
endapo watamuona mtu yeyote akiwanyanyasa au kuwafanyia ukatili wowote
watoto.
Post a Comment