Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MWANANCHI AMBAYE ANAKIDHI VIGEZO NA HATAJIANDIKISHA UPYA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA, KUTORUHUSIWA KUPIGA KURA

 

 Kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi jaji John Mkwawa akizungumza na waandishi wa habari wa mkoa wa Njombe kuhusu kupeleka elimu kwa jamii ili wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika daftari ya kudumu la wapiga kura kwa mfumo mpya.
======
Tume ya taifa ya uchaguzi imewataka wananchi wanaotakiwa kujiandikisha kupiga kura kwa mujibu wa sheria, kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo ili waweze kupiga kura ya maoni ya katiba mpya pamoja na uchaguzi mkuu 2015. 
Kauli hiyo imetolewa leo Julai mosi na Kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi Mh. Jaji John Mkwawa katika ufunguzi wa mkutano wa tume hiyo na waandishi wa habari mikoani uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya Njombe mkoani Njombe. 
Jaji Mkwawa amesema hata kama wananchi wamejiandikisha toka awali na wanavitambulisho, vitambulisho hivyo havitatumika tena na badala yake mwananchi mwenye umri wa miaka 18 au zaidi atatakiwa kujiandikisha upya kupitia teknolojia mpya ijulikanayo kama "Biometric Voter Registration"(BVR). 

Wandishi wa habari wakimsikiliza.
Mkurugenzi wa idara ya habari ya tume hiyo Bibi Ruth MashamHatua hiyo imefikiwa na tume ikiwa ni njia mojawapo itakayosaidia kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura ikiwemo kuwaondoa wale waliojiandikisha mara mbili, waliopoteza sifa kwa mujibu wa sheria, waliofariki, pamoja na wale watakao hama vituo kabla ya siku ya kupiga kura
Jaji huyo amewataka wananchi kujitokeza kujiandikisha upya hivi karibuni kwa kuwa kazi ya kuanza kuandikisha wapiga kura nchini itaanza kufanywa kwa jinsi tume ilivyojipanga, na yeyote aliye na sifa anatakiwa kushiriki kwani kwa sasa idadi ya vituo vya kujiandikisha vimeongezeka hadi kufikia ngazi ya vitongoji na mitaa ili kuwarahisishia wananchi.
 
Mkurugenzi wa idara ya habari ya tume ya taifa ya uch Bibi Ruth Masham akiongea na waandishi wa habari leo.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa idara ya habari ya tume hiyo Bibi Ruth Masham amesema tume hiyo kwa sasa imejipanga vilivyo kufikisha ujumbe huo kupitia waandishi wa habari kote nchini, huku akiwasisitiza wanahabari hao kufikisha elimu kwa jamii ili lengo la wananchi wote wenye sifa waweze kujiandikisha. 
Amesema matumizi ya mfumo huo mpya wa BVR utatumiwa kwa shughuli za uchaguzi tu na si vinginevyo ambapo alama zote za vidole 10 vya mikono, saini pamoja na picha ndivyo vitakavyochukuliwa wakati wa uandikishaji. 

"Zoezi hili linashirikisha wote wenye mika 18 na zaidi, wale wenye ulemavu mfano hawana vidole vyote upo utaratibu mzuri ulioandaliwa, wote watapatiwa vitambulisho.
 Mwanahabari Lilian Mkusa wa gazeti la daraja letu mkoani Njombe akiuliza swali
 Gabriel Kilamlya kutoka Uplands fm akiuliza swali lake.
Basil Makungu wa gazeti la mwananchi akiuliza maswali ya ufahamu kuhusu zoezi hilo
Wakijiandaa kujibu maswali
Waandishi hao wa habari mkoa wa Njombe walioshiriki katika mkutano huo wameahidi kushirikiana na tume ya taifa ya uchaguzi kufikisha ujumbe huo kwa jamii huku wakionesha kufurahishwa na tume kuwashirikisha mapema(kuwafanya watu wa kwanza) kukutana nao kabla ya wadau wengine
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top