Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

NAIBU WAZIRI AWAKALIA SHINGONI BODI YA PAMBA TANZANIZ!!!

 

Naibu waziri wa kilimo chakula na ushirika Godfrey Zambi (pichani) ametoa siku mbili kwa bodi ya pamba Tanzania kanda ya magharibi kuhakikisha inalimaliza mara moja tatizo la wakurugenzi wa halmashauri za wilaya katika mkoa wa Simiyu la kuyatoza ushuru makampuni ya kununua pamba ambao tayari unalipwa na serikali.
 
Agizo hilo amelitoa jana wakati wa majumuisho ya ziara yake ya siku mbili wilayani Kahama baada ya kuelezwa kuwa makampuni ya kununua pamba katika mikoa ya shinyanga na simiyu Mkoani Simiyu yamepata pingamizi kubwa la kutozwa ushuru ambao tayari serikali imeufuta.
 
Kabla ya hapo taarifa ya makampuni hayo ya kununua pamba katika mikoa hiyo iliyotolewa na meneja wa Kampuni ya Kahama Oil Mill ya mjini Kahama Wiliam Matonange imeeleza kuwa mkoani Simiyu halmashauri zote zimezuia pamba isinunuliwe bila kulipa Ushuru huo
 
Hali hiyo imemshangaza waziri Zambi ambaye amesema serikali tayari imetenga shilingi bilioni 10 kwa ajili ya kufidia shilingi 30 kwa kila kilo itakayonunuliwa fedha ambayo zitalipwa halmashauri zote zenye zao la  pamba kwa lengo la kufidia ushuru huo
 
Zambi alisema serikali iliona itoe fedha hiyo ili iyafanye makampuni yanunue zao hilo kwa shilingi 750 kwa kilo badala ya 720 kwa kilo kama yangeendelea kulipa ushuru huo katika halmashauri hizo.
 
Kufuatia hali hiyo waziri zambi alimuagiza mkurugenzi huyo wa bodi ya pamba Tanzania kanda ya magharibi Buluma Kalidushi kulimaliza tatizo hilo baada ya hapo atalifikisha kwa waziri mkuu aliyetoa agizo hilo la kufuta ushuru huo katika halmashauri za wilaya zenye zao la pamba
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top