CESARE
Prandelli amethibitishwa kuwa kocha mkuu wa klabu ya Galatasaray ya
Uturuki zikiwa zimepita wiki mbili tangu ajiuzulu kuifundisha timu ya
Taifa ya Italia kutokana na matokeo mabaya ya kombe la dunia nchini
Brazil.
Miamba hiyo ya Uturuki imeweka
taarifa rasmi kwenye mtandao wao wa klabu leo jumatatu, ikisema kuwa
kocha huyo mwenye miaka 56 atasaini mkataba wa miaka miwili kurithi
mikoba ya Roberto Mancini.
Prandelli atawasili Uturuki leo
jioni kabla ya kusaini mkataba, na kesho jumanne atatembelea uwanja wa
mazeozi pamoja na wachezaji.
Galatasaray walikuwa wakihusishwa kuzungumza na Prandelli tangu ajiuzulu kuifundisha Italia, huku David Moyes naye akihusishwa.
Prandelli atamrithi Mancini
katika dimba la Turk Telekom Arena kufuatia kocha huyo kuondoka kwa
makubaliano maalum mwezi juni ikiwa ni miezi tisa tangu aanze kazi hiyo.
Mkurugenzi wa michezo wa
Galatasaray, Tomas Ujfalusi, siku za karibuni alikiri kuwa ujuzi na
uzoefu wa Prandelli katika soka la Italia utasaidia kuendeleza kazi
aliyofanya Mancini klabuni hapo.
“Wakati Mancini anasema hataki kuendelea, nilataka kumleya Cesare,” Ujfalusi alikaririwa akizungumza na gazeti la Gazetta dello Sport.
Post a Comment