Manchester United lazima waguse mfuko kama wanataka kumsajili nyota wa Ureno William Carvalho.
Manchester
United imeambiwa kuwa inatatakiwa kulipa paundi milioni 37 kama inataka
kumsajili kiungo wa Sporting Lisbon, William Carvalho.
Man
United wamejaribu kuomba kupunguziwa bei wakati Chelsea nao wameonesha
nia ya kutaka kumsajili, lakini klabu hiyo ya Ureno imeonya kuwa
haitamuuza kwa bei rahisi.
Anazivutia klabu: Chelsea pia wameeleza kuvutiwa na nyota huyu wa Sporting.
Mkurugenzi
wa michezo wa Sporting, Augusto Ignacio alisema: "Sio kama miaka ya
nyuma wakati wachezaji wa Sporting walikuwa wanauzwa kwa bei yoyote.
Kuvunja mkataba kunaihakikisha Sporting dili kubwa. Nimevutiwa na
makubaliano".
Post a Comment