Kijana Lawrent Lawrian, akiwa na uvimbe wa ajabu kichwani mwake.
Lawrent
Lawrian, 42 (pichani), ni mkazi wa Kijiji cha Nyakisogo, Wilaya ya
Biharamlo, mkoani Kagera, amekuwa mwenye huzuni na kukosa raha kwa muda
wa miaka 35 kutokana na gonjwa la ajabu linalomtesa ambalo
limemsababishia mambo mengi ikiwa ni pamoja na kutoendelea na masomo.
Gonjwa
hilo la ajabu ni uvimbe kama nundu kichwani wenye uzito wa kilo 3,
ulimuanza akiwa darasa la kwanza.Akielezea zaidi kwa njia ya simu hivi
karibuni Lawrent alisema: “Gonjwa hili lilianza kama
kauvimbe nikiwa na umri wa miaka saba, wakati huo nilikuwa na wazazi
wote na ilipofika mwaka 1992 baba akafariki dunia. “Nikabakia na
mama tukawa tunaishi kwa kutegemea kilimo cha kawaida, nilikuwa nikienda
shule lakini ilifikia hatua nilishindwa kutokana na maumivu na
manyanyaso. “Darasa la saba nilimaliza kwa tabu sana, kwani
wanafunzi wenzangu walikuwa wakinicheka na kunitenga, licha ya
kuadhibiwa na walimu lakini hawakuacha tabia yao.“Kutokana na
hali hiyo, nilishindwa kuendelea na masomo kwani nilikuwa nikifungiwa
ndani ili kunipunguzia kero toka kwa wenzangu.SOMA ZAIDI>>>
Post a Comment